Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 24, 2013

ALHY NA ZAMALEK WAREJESHA WAKALI WAO KWA AJILI YA MCHEZO WA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Ahly na Zamalek wawarejesha wakali wao kwa ajili ya mchezo wao wa ligi ya mabingwa Afrika hapo kesho.Timu mbili pinzani katika soka la nchini Misri Al Ahlyna  Zamalek zinatarajia kuanza kampeni yao za kuwania taji la vilabu barani Afrika  baada ya kukutana na kukubaliana juu ya eneo na uwanja utakaotumika katika mchezo wao utakaochezwa hapo kesho. Vilabu vyote hivyo maskani yao ni katika jiji la Cairo, zitakuwa zikikutana katika mchezo wa ufunguzi wa kundi wa A huko katika uwanja wa El Gouna maeneo ya Red Sea.
Makubaliano juu ya uwanja utakao tumika yamefikiwa kutokana na sababu za kiusalama kutokana na nchini hiyo kukumbwa na hali isitulia kisiasa ambapo mchezo huo uliahirishwa wiki iliyopiya kutokana na sababu za kibiashara"marketing reasons".
Pande zote mbili zimewaita nyota wao muhimu katika sehemu ya kiungo akiwemo Mohamed Aboutrika kwa upande wa Ahly and Mahmoud Abdel Razak kwa upande wa  Zamalek.

Aboutrika, anatazamwa kama ni mmoja wa wachezaji wakubwa kabisa kuwahi kuchomza katika soka la ukanda wa Afrika Magharibi akiwa ameshakamilisha kipindi chake cha mkopo katika klabu ya Baniyas ya Falme za kiarabu.
Kiungo mwenye kipaji "volatile" Abdel Razak, akijulikana zaidi kama 'Shikabala', pia amekuwepo kwa mkopo huko falme za kiarabu katika klabu ya Al-Wasl miezi nane iliyopita.
Wote hawa ni wachezeshaji ambao wamekuwa wakifanya kazi ya kuendesha sehemu ya kiungo katika vilabu vyenye mafanikio makubwa barani Afrika katika michuano mikubwa ya Confederation na champions huku Ahly wakishinda mataji ya vilabu Afrika mara 16 nao Zamalek mara tisa.
Hata hivyo vikosi vyote vitawakosa wapiga mabao wao hodari Emad Moteab kwa upande wa Ahly mwenye majeraha na kwa upande wa Zamalek wao watamkosa Abdoulaye Cisse ambaye ameihama Zamalek.
Kutokana na sababu za kiusala kuwa ndogo kufuatia kuangushwa kwa utawala wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Mohamed Morsi mchezo huo sasa utapigwa katika uwanje wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 12,000 na usiokuwa na usiokuwa na taa za kutosha mchezo huo sasa utalazimika kuchezwa mchana kweupe.
Inaarifiwa kuwa hali hiyo itawasumbua sana wachezaji ambao wengi wao wako katika funga ya mwezi wa Ramadhani.
Licha ya kwamba wachezaji wa timu hizo wameruhusiwa kula na kunywa katika siku ya mchezo  lakini wengi wanaamini kuwa bado haitawajenga vizuri katika imani kutokana na imani ya dini zao

No comments:

Post a Comment