VINARA wa Ligi Kuu Yanga SC, wameingia kambini leo katika Hotel ya Tansoma kujiandaa na mechi yao ya jumatano dhidi ya Kagera Sugar mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa.
Akizungumza leo, Ofisa Habari wa klabu hiyo Baraka Kiziguto alisema kuwa, timu hiyo imeingia kambini kutokana na mapendekezo ya Kocha Mkuu Ernie Brandts.
Kiziguto alisema timu hiyo ikiwa kambini inaendelea na mazoezi ya katika Uwanja wa Bora Kijitonyama, na baada ya mechi hiyo watasikiliza tena maamuzi ya Kocha kama kuendelea na kambi hiyo au la.
"Timu imeingia kambini kutokana na mapendekezo ya Kocha kujiandaa na mechi ya keshokutwa (kesho), na baada ya hapo Kocha ataamua kuendelea kukaa hapo au la," alisema Kiziguto.
Aliongeza kuwa Kocha alitoa maamuzi hayo kutokana na kuwa Ligi Ngumu kwa sasa kwani kila timu inajiandaa kufa na kupona katika hatua za kuelekea mwishoni.
Yanga ipo katika nafasi ya kwanza ya Ligi hiyo ikiwa na pointi 39, inatarajia kushuka dimbani kesho katika mechi yake dhidi ya Kagera Sugar.
DIRA YA TAIFA YA 2050 KUIKIJANISHA TANZANIA
-
Mwanandishi wetu, Morogoro.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Masauni amesema
Usimamizi na uhifadhi wa mazingira hauwezi kufani...
Africa, Redefined: Mobila Safaris at Indaba 2026
-
The wait is over. Africa’s most iconic landscapes are calling, and we’re
here to hand you the keys.
*Mobila Safaris is officially live at Stand DEC...
KUMBUKIZI YA DARAJA LA NYERERE 2016-2026
-
Daraja la Nyerere lililozinduliwa na aliye kuwa Rais wa Tanzania John
Pombe Magufuli Aprili 19, 2016. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Picha za Viongozi mba...
WASIRA AWATOLEA UVIVU WALIOANZA MBIO ZA URAIS
-
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Stephen
Wasira, Leo Machi 27, 2026, Mjini Bunda Mkoa wa Mara alipokuwa akiweka
jiwe la ms...
Post a Comment