Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, February 25, 2013

NEW HABARI YAANZA KUJIWINDA MASHINDANO YA VYOMBO VYA HABARI YANAYODHAMINIWA NA NSSF


TIMU ya New Habari FC inatarajia kuanza mazoezi rasmi kesho kwa ajili ya kuajiandaa na Mashindano yanayoandaliwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), itakayoanza Machi 9 kwenye Uwanja wa TCC Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa New Habari FC, Mohamed Mharizo, amesema mazoezi hayo yatafanyika kwenye uwanja wa Shule ya Mugabe kuanzia saa kumi alasiri.

“Tunaanza mazoezi Jumatano kwa ajili ya mashindano ya NSSF Cup, hivyo wachezaji wote wanatakiwa kufika uwanjani bila kukosa,” alisema Mharizo.

Alisema kabla ya kuanza kwa mashindano hayo, watacheza mechi moja ya kirafiki, kwa ajili ya kuajiandaa na mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment