Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 2, 2017

PSG YAINGIA MATATANI, KUCHUNGUZWA NA UEFA

KLABU ya Paris St Germain ya nchini Ufaransa imelishtua shirikisho la soka barani Ulaya (UEFA) baada ya kumsajili kinda Kylian Mbappe kwa dau kubwa ikiwa ni  wiki chache baada ya kuvunja rekodi kwa kumsajili Neymar kwa gharama ya paundi 198 milioni.
Katika dili la Mbappe, PSG walikuwa na nafasi ya kuchagua aidha kumchukua kwa mkopo au kumsajili lakini imeonekana ni lazma kwa Monaco kuwauzia kinda huyo kwa paundi 166 milioni 2018 majira ya joto na kufanya usajili huo kuwa wa pili katika rekodi za usajili.
Mbappe amejiunga na PSG kwa mkopo
Chombo hicho kikubwa cha mpira wa miguu barani Ulaya kilitoa taarifa kuwa “Kamati ya UEFA ya uchunguzi na Udhibiti wa Fedha za klabu imefungua uchunguzi rasmi juu ya Paris St Germain kama sehemu ya ufuatiliaji unaoendelea wa klabu chini ya kanuni ya kifedha ya Financial Fair Play (FFP)”
Nasser Al-Khelaifi ambaye ni mwenyekiti wa Paris St Germain alinukuliwa akisema “Kama una wasiwasi kuwa klabu yangu imekiuka taratibu za usajili wa Neymar inakupasa utulie na kunywa kahawa kwani hakuna tatizo”
FFP ilianzishwa ili kulinda uchumi wa klabu mbalimbali ziweze kutumia fedha kutokana na mapato yanayopatikana na kutotumia fedha zitokanazo na mfuko wa mmiliki wa klabu.

No comments:

Post a Comment