Katika dili la Mbappe, PSG walikuwa na nafasi ya kuchagua aidha kumchukua kwa mkopo au kumsajili lakini imeonekana ni lazma kwa Monaco kuwauzia kinda huyo kwa paundi 166 milioni 2018 majira ya joto na kufanya usajili huo kuwa wa pili katika rekodi za usajili.

Mbappe amejiunga na PSG kwa mkopo
Nasser Al-Khelaifi ambaye ni mwenyekiti wa Paris St Germain alinukuliwa akisema “Kama una wasiwasi kuwa klabu yangu imekiuka taratibu za usajili wa Neymar inakupasa utulie na kunywa kahawa kwani hakuna tatizo”
FFP ilianzishwa ili kulinda uchumi wa klabu mbalimbali ziweze kutumia fedha kutokana na mapato yanayopatikana na kutotumia fedha zitokanazo na mfuko wa mmiliki wa klabu.
No comments:
Post a Comment