GEORGE
Lwandamina ameanza kuonesha ubora kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania
Bara, baada ya Yanga kutoka nyuma na kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya
Singida United katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Katika mchezo
huo wa kirafiki, Singida, ndiyo walioutawala mchezo huo kwa asilimia kubwa na
kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-1.
Kiungo
Mzimbabwe, Thabani Kamusoko alikuwa wa kwanza kuifungia Yanga bao la kuongoza
dakika ya tano baada ya kupiga mpira wa faulo, ulikwenda moja kwa moja wavuni
na dakika tatu baadaye, Dany Usengimana akaisawazishia Singida United bao
akiunganisha kwa kichwa krosi ya Deusi Kaseke.
Mshambuliaji
Mzimbabwe, Simbarashe ‘Simba’ Nhivi Sithole akaifungia bao la pili Singida
katika dakika ya 23 akitumia tena makosa ya safu ya ulinzi ya Yanga na kufanya
matokeo kubaki hivyo hadi mapumziko.
Kipindi cha
pili Yanga iliwatoa baadhi ya wachezaji wake wenye majina makubwa kama akina
Donald Ngoma, Nadir Haroub Cannavaro, Kelvin Yondan, Thaban Kamusoko na Beno
Kakulani na kuendelea kupambana ili kusawazisha mabao hayo, lakini walikuwa ni
Singida United walioonekana kucheza kwa kuelewana na kuwapoteza Yanga.
Mambo
yalianza kuwabadilikia Singida dakika ya 83, baada ya Amissi Tambwe,
kuisawazishia timu yake bao kwa mkwaju wa penalti baada ya kipa Said Lubawa
kumuangusha kwenye eneo la hatari Mussa Abdallah.
Bao hilo
lilionekana kuwazindua mashabiki wa Yanga, ambao kwa muda mrefu walionekana
kutoridhishwa na kiwango kinachooneshwa na timu yao hususani baada ya kutoka
kwa wachezaji wenye majina makubwa.
Dakika ya 90
Martin alimaliza mchezo kwa kuifungia Yanga bao la ushindi kufuatia shuti kali
la mbali ambalo lilimshinda kipa wa Singida United na mpira kujaa wavuni.
Katika
mchezo huo Singida United ilipoteza penalti mbili zilizotolewa na mwamuzi
Martin Saanya, huku Yanga ikiutumia
vizuri mkwaju huo kupitia kwa Tambwe.
Kiujumla
Yanga haikuonyesha kiwango kikubwa sana hasa wachezaji wageni ambao ndiyo macho
ya wengi yalikuwa yakiwafuatilia.
Huo ni
mchezo wa saba wa majaribio kwa Singida United bila kushinda bada ya hivi
karibuni kufungwa na wenzao walipanda daraja wa Lipuli ya Iringa.
Wakati
huohuo, Yanga imefanikiwa kuinasa saini ya beki wa kushoto wa Azam FC, Gadiel
Michael baada ya viongozi wa timu hiyo kumalizana na timu hiyo.
Msemaji wa
Azam FC, Jafari Idd Maganga, alisema wanamtakia kila la kheri kwenye maisha
yake mapya akiwa na kikosi cha Yanga
Kikosi cha
Yanga ; Beno Kakolanya/Youth Rostand, Juma Abdul, Hajji Mwinyi/Hassan Kessy,
Kevin Yondan/Andrew Vincent ‘Dante’, Nadir Haroub ‘Cannavaro’/Abdallah Hajji
‘Ninja’, Thabani Kamusoko, Pius Buswita/Emmanuel Martin, Raphael Daudi/Juma
Mahadhi, Donald Ngoma/Amiss Tambwe, Ibrahim Hajib/Said Juma na Baruan
Akilimali.
Singida
United; Said Lubawa, Michael Rusheshagonga, Shafiq Batambuze, Elisha Muroiwa,
Juma Kennedy, Mudathir Yahya, Deus Kaseke, Tafadzwa Kutinyu, Nhivi Simbarashe,
Danny Usengimana na Kigi Makasi.
No comments:
Post a Comment