Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, May 14, 2017

XHAKA, RAMSEY UNAVYOING’ARISHA ARSENAL, AWAFUMBA MIDOMO WAKOSOAJI

Image result for xhaka


GRANIT Xhaka hatamaye sasa anaonekana kama mchezaji mwenye thamani ya pauni milioni 30 ambayo kocha wa Arsenal Arsene Wenger alitumia kumsajili nyota huyo wakati wa majira ya kiangazi akitokea Borussia Monchengladbach .
Xhaka tangua ameanza kucheza na kiungo wa kimataifa wa Wales Aaron Ramsey katika eneo la kiungo cha Arsenal wameonekana kuunda ushirikiano mzuri na sasa anaonekana kuendana na dau la pauni milioni 30 lililotumika kumtwaa.
Wakati Arsene Wenger alipomuelezea Granit Xhaka kama aina ya mchezaji mwenye uwezo wa kucheza kama kiungo cha chini na cha juu mwanzoni mwa msimu inawezekana hakuna mtu aliyechanganywa na kauli hiyo ya profesa zaidi ya Xhaka mwenyewe.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 sio mtu mwenye uwezo wa kujitengenezea nafasi na kuwatoka mabeki, huku tamko hilo la Wenger likionekana kama la majaribio zaidi ingawa kwa sasa hakuna mwenye shaka tena kama kiungo huyo wa kimataifa wa Uswisi anauwezo mkubwa wa kwenda mbele kushambulia lakini wakati huo huo kutekeleza majukumu yake kama kiungo mkabaji na ndicho kinachotokea kwa Arsenal kwa sasa.
Miezo miwili baadae, Wenger aliikana kauli yake ya kuwa Xhaka ni aina ya kiungo mwenye uwezo wa kucheza sehemu ya ulinzi na kiungo cha ushambuliaji kwa kusema kuwa ni aina ya kiungo mpiga pasi zaidi kuliko uwezo wa kuwatoka mabeki na kutengeneza nafasi.
“Granit ni aina ya kiungo kinachofanya shughuli zake kuanzia eneo la chini ya uwanja kuliko kukaba na kwenda mbele kushambulia ,” alisema Wenger.


“Haonekani kwenye eneo la mwisho la maadui mara nyingi. Ni aina ya mchezaji mwenye pasi za uhakika kupitisha katikati ya wapinzani.“Anapata mpira kutoka kwa mabeki na kuwatafuta viungo wa juu kwa pasi ndefu. Faida yake ni uwezo wa kile tunachokiita pasi za wastani-pasi zinazotoka kwa kiungo wa chini kwenda kwa viungo wa juu.”
Huku msimu ukielekea ukingoni sasa tunaanza kumuona Xhaka kwenye majukumu aliyoyatumikia kwenye maisha yake yote ya soka.
Kiungo huyu wa kimataifa wa Uswisi ni aina ya mchezaji anayefanya mambo yatokee kwa pasi zake za uhakika na maono kwenye pasi zake maana yake ni hadhina kubwa kwa Arsenal zaidi ya hasa akipata muda na nafasi katika eneo la katikati.
Kwenye mechi za karibuni zimeonyesha faida ya kuwatumia Aaron Ramsey na Xhaka kwani hiyo inampa uhuru zaidi kiungo huyo wa zamani wa Borussia Monchengladbach kuuona mchezo toka eneo la chini.
Ushirikiano mzuri wa Ramsey na Xhaka ulionekana wazi dhidi ya Southmpton ambapo viungo hao wawili kwa ujumla wao waligusa mpira mara 154 sawa na asilimia 89.5 ya pasi za uhakika kwenye mechi hiyo huku wakichukua mpira toka kwa wapinzani mara 14-walipiga pasi nyingi zaidi, walizunguka eneo kubwa zaidi lakini pia waligusa mpira mara nyingi zaidi.
Haitaonekana kama inakuzwa sana ikisemwa Ramsey anakimbia zaidi na Xhaka ni kama mafuta kwenye injini ya kiungo huyo wa kimataifa wa Wales.
 “Tunazoeana mechi hadi mechi na kwa sasa inaonekana kuzaa matunda, hasa katika ulinzi inaonekana imara sana,” alisema Wenger akisifu mabadiliko ya mfumo kwenye timu yake.
 “Lakini kitu muhimu zaidi kwenye mfumo huu ni kwamba unaendana na ubora wa wachezaji. Ramsey ni mzuri sana kujilinda nyuma yake na ana uhuru zaidi kwenda mbele na kuingia eneo la penalty.

“Akiwa katika ubora wake kimwili, anakuwa injini kubwa. Ana makadirio mazuri kwenye kukimbia kwake, anapokuwa sawa kimwili anatumia faida ya mbinu alizokuwa nazo kwenye mchezo wake.“
TXhaka-Ramsey wamecheza dakika 783 pamoja msimu huu na katika kipindi hicho Arsenal imefunga mabao 22 na kuruhusu mabao manane. Mabadiliko ya kimfumo ya Wenger yanamuwezesha Ramsey kuwa na nafasi ya kutosha kwenda mbele na kushuka chini na kasi yake kwenye eneo la mwisho la maadui ni marejeo ya kiwango alichoonyesha kwenye fainali za Mataifa ya Ulaya mwaka 2016 akiwa na timu ya taia ya Wales.
Ni muhimu ushirikiano huu wa eneo la kiungo Arsenal ukaendelea hadi msimu ujao kama tulivyoona miaka iliyopita jinsi gani ilivyo muhimu kwa eneo la kiungo kutawala mchezo.
Majeruhi ya Santi Cazorla yamemfanya Ramsey kutumia nafasi yake vizuri kucheza sambamba na Xhaka katika eneo la kiungo na ushirikiano wao unaonekana kuimarika mechi hadi mechi.
Hatimae Arsenal imepata ushirikiano mzuri waliousubiri kwa muda mrefu katika eneo la kiungo na wale ambao walisema Xhaka haendani na aina ya uchezaji wa Arsenal watakula maneno yao. Kiasi cha pauni milioni 30 kilichotumika kumsajili kiungo wa umri wa miaka 23 ambae anaanza kuimarika sio fedha nyingi kabisa.

No comments:

Post a Comment