Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, May 20, 2017

CHIN BEES AACHIA WIMBO NA VIDEO MPYA ‘NYONGA NYONGA’






Dar es Salaam, May 20, 2017,

Baada ya kujitengenezea heshima adimu kama ‘Prince wa Trap’ Tanzania kupitia ngoma yake, Pepeta, Chin Bees ameachia wimbo mpya ‘Nyonga Nyonga’ pamoja na video yake.

Wimbo huo wenye mahadhi ya dancehall iliyochanganyikana na ladha za aina yake za Kibongo, unadhihirisha uwezo wa Chin katika kubadilika kwenye mahadhi mbalimbali kama atakavyo. Nyonga Nyonga ambao ni wimbo wa pili wa rapper huyo akiwa chini ya usimamizi wa label ya Wanene Entertainment.

 “Ni dancehall lakini za watu fulani ambao wamezimiss. Ni muziki fulani tofauti ambao hata mtu akisikiliza lazima atabounce,” anasema. Ameongeza, “It’s a typical African hit na ikishakuwa hivyo inaweza kusikilizwa kokote Afrika kwasababu nilichokifanya ni vitu ambavyo viko musical, kote duniani wanaweza wakafeel. It’s a new tone,” anasema.

“Nimewaletea watu kitu ambacho ni tofauti ambacho kitawafanya wacheze na mind zao ziwe fresh kwa kusikiliza.”
Wimbo huo umetayarishwa na Dr.Reggy, mpishi ambaye amewahi kufanya miradi mingi na Chin Bees siku za nyuma. “Dr.Reggy ni producer wangu wa kwanza kabisa, nimeanza kufanya naye kazi kitambo kabla hata sijawa na jina kubwa,” anafafanua.

Video ya wimbo huo imefanyika katika mitaa mbalimbali ya Dar es Salaam huku rangi za nguo walizovaa wote wanaoonekana, zikitengeneza picha ya kuvutia machoni na yenye Uafrika mwingi.
Kuhusiana na video hiyo Chin amesema, “Imefanyika hapa hapa Wanene na tuliamua kuifanyia nje zaidi tofauti na video yangu iliyopita ya Pepeta ambayo yote ilifanyika ndani. Tumefanya kwenye yale mazingira ya mtaani kabisa.”

“Theme ya video ilikuwa ni kuonesha rangi za mtaani na mavazi pamoja na mazingira halisi ya Kitanzania na yenye muonekano wa kizamani,” anasema Director H aliyeiongoza video hiyo.
Nguo hizo zimebuniwa na mbunifu wa mavazi, Samuel Sebedayo (SAMZ) huku Rehema Samo akihusika kwenye styling.

Nyonga Nyonga ni wimbo unaotarajiwa kuwa katika albamu ya kwanza ya Chin Bees iliyopangwa kuachiwa baadaye mwaka huu.

Kuangalia video ya Nyonga Nyonga, bofya hapa: https://www.youtube.com/watch?v=-z0HGHpMEwo&feature=youtu.be
Kupakua wimbo bofya hapa: http://bit.ly/NyongaNyonga

KUHUSU CHIN BEES

Chin Bees ni rapper mwenye asili ya Arusha aliyejizolea umaarufu kwa kipaji chake si tu katika kurap, bali pia kuimba nyimbo za aina mbalimbali. Pamoja na nyimbo zake zikiwemo Pepeta, Zuzu, Pakaza, Ruba na zingine kufanya vizuri redioni na kwenye runinga, ameshirikishwa kwenye ngoma za  wasanii wakubwa wakiwemo Nick wa Pili na kushiriki kuandika nyimbo za wasanii kama Navy Kenzo na Vanessa Mdee. Yuko chini ya usimamizi wa label ya Wanene Entertainment

KUHUSU WANENE ENTERTAINMENT

Wanene Entertainment kampuni ya utayarishaji wa maudhui yenye studio za kisasa zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na yenye makazi yake jijini Dar es Salaam. Imejikita katika utengenezaji wa maudhui ya sauti, video na picha kwa kutumia wataalam waliobobea katika sekta hiyo. Wanene imedhamiria kuleta mapinduzi katika burudani kwa kutayarisha bidhaa zenye kiwango cha kimataifa.


No comments:

Post a Comment