Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, May 29, 2017

Arsenal yamuweka sawa Sanchez



Related image
LONDO, England
ARSENAL imeweka ofa nyingine mezani kumbakisha nyota wake Alexis Sanchez anayesakwa na Bayern Munich.
Mkataba huo unafahamika ni wa mshahara wa pauni 270,000 kwa wiki, ambao ni kidogo kulinganisha na kiasi cha pauni 300,000 kwa wiki anachotaka mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Chile, ingawa ofa hiyo ina marupurupu mengi ambayo inakaribia kufikia pauni 300, 000 wanazotaka.
Bayern inatajwa kumuwania Sanchez kama atakataa kusaini mkataba mpya na Arsenal, wakati huu wa majira ya kiangazi, lakini pia klabu za Juventus na Paris Saint-Germain zinamuwania mshambuliaji huyo.
Uvumi ulizagaa wiki hii kuwa ameshafanya uamuzi baada ya Chama cha Soka cha Chile kumuorodhesha kwa bahati mbaya kwenye kikosi cha timu yao kuwa mshambuliaji huyo anatokea Bayern Munich.
Alex Oxlade-Chamberlain pia anatarajia kuanza mazungumzo ya mkataba mpya baada ya fainali za Kombe la FA. Chamberlain yuko mwaka wa mwisho wa mkataba wake na Liverpool inatajwa kumuwania winga huyo.

No comments:

Post a Comment