Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, April 7, 2017

WANAWAKE WATAKIWA KUJIAMINI KATIKA MICHEZO





SERIKALI imewahimiza wanawake viongozi wa michezo nchini kuondokana na unyonge na kujiamini kwa uwezo wa kufikiri ili wapate kuheshimika.
Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel wakati akifungua kongamano la wanawake na michezo lililoandaliwa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT).
Nasikitika kuwaona akina mama ni wanyonge. Msipojiamini hata muwe na mabilioni kiasi gani haisaidii. Mjiamini kwa uwezo wa kufikiri,alisema.
Pia, alizungumzia ubunifu  katika vyama au klabu wanazoziendesha ulenge kutoa michango yao kwa watu wanaowaongoza na kujiepusha kuwa sehemu ya migogoro au matatizo.
Alisema yapo matatizo mengi yanaweza kutatuliwa kwa njia ya michezo, kwa kuwa michezo ni umoja na hushirikisha watu wa matabaka mbalimbali bila kujali itikadi zao za kisiasa wala dini.
Professa Gabriel alisema serikali iko pamoja nao hivyo, wanachotakiwa kufanya wanawake hao ni kusimamia utakelezaji wa mambo watakayoazimia.
Aliomba wadhamini mbalimbali kuwasaidia wanawake katika michezo yao kwani wamekuwa wakiwakilisha vyema.
Kwa upande wake, Mjumbe wa BMT Jennifer Shanga alisema mwanamke ili aweze kuleta mabadiliko anatakiwa kujiamini mwenyewe kwa kuhakikisha anakuwa ni Kocha mzuri kabla ya kuwafundisha wengine.
Alisema kuna umuhimu mkubwa wa kutekeleza tamko la Brighton linalotoa mwito kwa taasisi zote binafasi na serikali  kushiriki katika maendeleo ya michezo.

No comments:

Post a Comment