Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, January 14, 2017

FAINALI ZA AFCON 2017:Nyota watakaokosa mechi za Ligi Kuu England



WAKATI mashindano ya Mataifa ya Afrika yakianza leo nchini Gabon, swali kubwa linaulizwa katika Ligi Kuu ya England ni timu gani iliyoathirika zaidi baada ya wachezaji wengi kwenda katika mashindano hayo?
Wakati tayari mataifa 16 ya Afrika yakiwa yamethibitisha vikosi vyao vitakavyoshiriki mashindano hayo, tunaangalia wachezaji gani wa Ligi Kuu ya England watakuwa Gabon kuanzia leo Jumamosi Januari 14 hadi Februari 5.
Wachezaji watakaokuwa Gabon watazikosa timu zao kwa takribani mechi nne za Ligi Kuu na hivyo baadhi ya timu kuathirika na kutokuwepo kwa wachezaji hao.

ARSENAL

Arsenal wenyewe katika Ligi Kuu ya England watamkosa mchezaji wao mmoja, Mohamed Elnery, ambaye yuko Gabon akiwa na nchi yake ya Misri.

BOURNEMOUTH
Timu hii itamkosa mchezaji wake mmoja, Max Gradel ambaye anaichezea timu ya taifa ya Ivory Coast, ambao ni mabingwa watetezi wa Afcon.

BURNLEY
Klabu hii ya Ligi Kuu yenyewe haina mchezaji yeyote anayeshiriki katika mashindano hayo ya Afcon, hivyo itakuwa na kikosi chake kamili wakati wote.

CHELSEA
Chelsea ambayo inaongoza katika msimamo wa Ligi Kuu ya England, yenyewe inaweza kuendeleza makali yake katika ligi hiyo kwani haina mchezaji yeyote Afcon.

CRYSTAL PALACE
Klabu hii itakosa huduma za wachezaji wake wawili, ambao ni Bakary Sako anayeichezea timu ya taifa ya Mali pamoja na Wilfried Zaha, ambaye anaichezea Ivory Coast.

EVERTON
Everton wenyewe watakosa huduma za mchezaji wao, Idrissa Gueye anayeichezea timu ya taifa ya Senegal.

HULL CITY
Klabu hii itakosa huduma za wachezaji wake, Ahmed Elmohamady anakipiga Misri pamoja na Dieumerci Mbokani anayeichezea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

LEICESTER CITY
Hawa ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England, ambao sasa watawakosa wachezaji wao watatu, ambao ni Riyad Mahrez, Islam Sliman, ambao wote wanaichezea Algeria pamoja na Daniel Amertey anayeichezea Ghana, Black Stars.

LIVERPOOL
Klabu ya Liverpool itamkosa mchezaji wake Sadio Mane anayeichezea timu ya taifa ya Senegal.

MAN CITY
Klabu ya Manchester City haina mchezaji yeyote anayeshiriki katika Afcon Gabon, hivyo itakuwa na kikosi chake kamili katika mechi zote za Ligi Kuu ya England.

MAN UNITED
Man United watamkosa Eric Bailly, ambaye anaichezea timu ya taifa ya Ivory Coast.

MIDDLESBROUGH
Haina mchezaji yeyote anayeshiriki fainali za Mataifa ya Afrika nchini Gabon.

SOUTHAMPTON
Hawana mchezaji yoyote nchini Gabon.

STOKE CITY
Klabu hii huenda ikaathirika zaidi baada ya kuwakosa wachezaji wake watatu, ambao watakuwa nchini Gabon wakishiriki na timu zao za taifa.
Wachezaji itakayowakosa ni pamoja na Mame Diouf wa Senegal, Ramadhani Sobhi wa Misri pamoja na Wilfred Bony wa timu ya taifa ya Ivory Coast.

SUNDERLAND
Sunderland itawakosa wachezaji watatu, hivyo inaweza kuathirika zaidi katika mechi zake za Ligi Kuu.
Klabu hiyo itawakosa Wahbi Khazri anayeichezea timu ya taifa ya Tunisia, Lamine Kone wa Ivory Coast na Didier Ndong.

SWANSEA
Klabu hii haina mchezaji yoyote Afcon Gabon 2017

TOTTENHAM HOTSPUR
Klabu hii nayo haina mchezaji yoyote Afcon 2017.

WATFORD

Watford itamkosa mchezaji wake mmoja, ambaye ni Adlene Guedioura anayeichezea timu ya taifa ya Algeria.

WEST BROMWICH ALBION
Haina mchezaji yoyote katika fainali za Afcon 2017.

HAM UNITED
Klabu hii itakosa huduma za wachezaji wake wawili, Andre Ayew wa Ghana na cheikhou Kouyate wa Senegal.
------
Vijue vikosi kamili:
Kundi A
BURKINA FASO
Makipa: Moussa Germain Sanou (Beauvais, Ufaransa), Herve Koffi (ASEC Mimosas, Ivory Coast), Aboubacar Sawadogo (RC Kadiogo, Burkina Faso)
Mabeki: Patrick Malo (Smouha, Misri), Issoufou Dayo (RC Berkane, Morocco), Bakary Kone (Malaga, Hispania), Issouf Paro (Santos, Afrika Kusini), Steeve Yago (Toulouse, Ufaransa), Souleymane Kouanda, (ASEC Mimosas, Ivory Coast), Yacouba Coulibaly (RC Bobo, Burkina Faso)
Viungo: Charles Kabore (Krasnodar, Russia), Prejuce Nacoulma (Kayserispor, Uturuki), Alain Traore (Kayserispor, Uturuki), Bertrand Traore (Ajax, Uholanzi), Cyrille Bayala (Sheriff Tiraspol, Moldova), Bakary Sare (Moreirense, Ureno), Blati Toure (Omonia, Cyprus), Adama Guira (Lens, Ufaransa), Abdoul Razack Traore (Karabuspor, Uturuki), Jonathan Zongo (Almeria, Hispania)
Washambuliaji: Jonathan Pitroipa (Al Nasr/UAE), Aristide Bance (ASEC Mimosas, Ivory Coast), Banou Diawara (Smouha, Misri).

CAMEROON

Makipa: Fabrice Ondoa (Sevilla, Spain), Jules Goda (AC Ajaccio, France), Georges Mbokwe (Coton Sport de Garoua, Cameroon).

Mabeki: Ernest Mabouka (MSK Zilina, Slovakia), Nicolas Nkoulou (Lyon, France), Ambroise Oyongo (Montreal Impact, Canada), Mohamed Djeitei (Nastic Tarragone, Spain), Fai Collins (Standard Liege, Belgium), Michael Ngadeu Ngadjui (Slavia Prague, Czech Rep), Adolphe Teikeu (Sochaux, France), Jonathan Ngwem (FC Progresso, Angola).

Viungo: Sebastien Siani (Ostende, Belgium), Georges Mandjeck (Metz, France), Arnaud Djoum (Hearts), Franck Boya (Apejes, Cameroon).

Washambuliaji: Vincent Aboubakar (Besiktas, Turkey), Benjamin Moukandjo (Lorient, France), Jacques Zoua (Kaiserslautern, Germany), Edgar Salli (Saint-Gall, Switzerland), Karl Toko-Ekambi (Angers, France), Clinton Njie (Marseille, France), Robert Ndip Tambe (Spartak Trnava, Slovakia), Christian Bassogog (Aalborg).

GABON

Makipa: Didier Ovono (KV Ostende, Ubelgiji), Yves Stephane Bitseki Moto (CF Mounana, Gabon), Anthony Mfa Mezui (hana timu).
Mabeki: Lloyd Palun (Red Star, Ufaransa), Andre Biyogho Poko (Kardemir Karabukspor, Uturuki), Aaron Appindangoye (Stade Lavallois, Ufaransa), Franck Perrin Obambou (Stade Mandji, Gabon), Bruno Ecuele Manga (Cardiff City), Yoann Wachter (CS Sedan Ardennes, Ufaransa), Johann Serge Obiang (ESTAC Troyes, Ufaransa), Benjamin Ze Ondo (Mosta FC, Malta).

Viungo: Junior Serge Martinsson Ngouali (IF Brommapojkarna, Sweden), Levy Clement Madinda (Nastic Tarragona, Hispania), Guelor Kanga Kaku (Etoile Rouge de Belgrade, Serbia), Merlin Tandjigora (Meixian Hakka FC, China), Didier Ibrahim Ndong (Sunderland), Samson Mbingui (Raja Casablanca, Morocco), Mario Rene Junior Lemina (Juventus, Italia).
Washambuliaji: Pierre Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund, Ujerumani), Malick Evouna (Tianjin Teda FC, China), Denis Athanase Bouanga (Tours FC, Ufaransa), Serge Kevyn Aboue Angoue (Uniao Leiria, Ureno), Cedric Ondo Biyoghe (CF Mounana, Gabon).

GUINEA-BISSAU
Makipa: Jonas Mendes (Salgueiros, Ureno), Rui Dabo (Cova da Piedade, Ureno), Papa Massé Mbaye Fall (Aguadulce, Hispania)
Mabeki: Emmanuel Mendy (Ceahlaul, Romania), Rudinilson Silva (Lechia Gdansk, Poland), Juary Soares (Mafra, Ureno), Agostinho Soares (Sporting Covilha, Ureno), Mamadu Candé (Tondela, Ureno), Eridson Mendes Umpeça (Freamunde, Ureno)
Viungo: Nani Soares (Felgueiras, Ureno), Jose Mendes Lopes Zezinho (Levadiakos, Ugiriki), Bocoundji Ca (Reims, Ufaransa), Tony Silva Brito (Levadiakos, Ugiriki), Toni Silva (Levadiakos, Ugiriki), Piqueti Djassi Brito (Braga), Idrissa Camara (Avellino, Italia), Jean Paul Mendy (US Quevilly-Rouen, Ufaransa), Francisco Santos Junior (Stromsgodset, Norway), Lassana Camara Sana (Académico de Viseu, Ureno)

Washambuliaji: Joao Mario Fernandes (Chaves, Ureno), Abel Issa Camara (Belenenses, Ureno), Amido Balde (CS Marítimo, Ureno), Frederic Mendy (Ulsan Hyundai, Korea Kusini)
Kundi B

ALGERIA

Makipa: Rais Ouhab M'bolhi (Antalyaspor, Uturuki), Malik Asselah (JS Kabylie, Algeria), Chemseddine Rahmani (MO Bejaia, Algeria).
Mabeki: Mokhtar Belkhiter (Club Africain, Tunisia), Mohamed Rabie Meftah (USM Alger, Algeria), Aissa Mandi (Real Betis, Hispania), Hicham Belkaroui (Esperance, Tunisia), Liassine Cadamuro (Servette Geneva, Uswisi) , Mohamed Benyahia (USM Alger, Algeria), Ramy Bensebaïni (Stade Rennes, Ufaransa), Faouzi Ghoulam (Napoli, Italia), Djamel Eddine Mesbah (FC Crotone, Italia).

Viungo: Adlene Guedioura (Watford), Saphir Taider (Bologna, Italia), Nabil Bentaleb (Schalke 04, Ujerumani), Mehdi Abeid (Dijon, Ufaransa), Yassin Brahimi (FC Porto, Ureno), Rachid Ghezzal (Olympique Lyon, Ufaransa).
Washambuliaji: Islam Slimani (Leicester City), Riyad Mahrez (Leicester City), Hilal Soudani El Arabi (Dinamo Zagreb, Croatia), Baghdad Bounedjah (Al Sadd, Qatar), Sofiane Hanni (Anderlecht, Ubelgiji).

SENEGAL
Makipa: Khadim N'Diaye (Horoya AC, Guinea), Abdoulaye Diallo (Caykur Rizespor, Uturuki), Pape Seydou N'Diaye (ASC Niarry Tally).

Mabeki: Lamine Gassama (Alanyaspor, Uturuki), Cheikh M'Bengue (Saint-Etienne, Ufaransa), Kara Mbodj (Anderlecht, Ubelgiji), Zargo Toure (Lorient, Ufaransa), Kalidou Koulibaly (Napoli, Italia), Saliou Ciss (Valenciennes, Ufaransa).
Viungo: Idrissa Gana Gueye (Everton), Cheikhou Kouyate (West Ham), Cheikh N'Doye (Angers, Ufaransa), Papakouli Diop (Espanyol, Hispania), Henri Saivet (Saint-Etienne, Ufaransa), Papa Alioune Ndiaye (Osmanlispor, Uturuki), Mohamed Diame (Newcastle).
Washambuliaji: Sadio Mane (Liverpool), Keita Balde Diao (Lazio, Italia), Moussa Konate (FC Sion, Uswisi), Famara Diedhiou (Angers, Ufaransa), Mame Biram Diouf (Stoke City), Ismaila Sarr (Metz, Ufaransa), Moussa Sow (Fenerbahce, Uturuki).

TUNISIA
Makipa: Aymen Mathlouthi (Etoile du Sahel, Tunisia), Rami Jridi (Club Sportif Sfaxien, Tunisia), Moez Ben Chrifia (Esperance de Tunis, Tunisia).
Mabeki: Ali Maaloul (Al Ahly, Misri), Hamza Mathlouthi (CS Sfaxien, Tunisia), Syam Ben Youssef (Caen, Ufaransa), Mohamed Ali Yacoubi (Caykur Rizespor, Uturuki), Aymmen Abdennour (Valencia, Hispania), Chamseddine Dhaouadi (Esperance Tunis, Tunisia), Slimane Kchok (Club Athletic Bizertin, Tunisia), Hamdi Nagguez (Etoile, Tunisia), Zied Boughattas (Etoile, Tunisia).

Viungo: Ferjani Sassi (ES Tunis, Tunisia), Larry Azouni (Nimes Olympique, Ufaransa), Naim Sliti (Lille, Ufaransa), Whabi Khazri (Sunderland), Mohamed Amine Ben Amor (Etoile, Tunisia), Ahmed Khalil (Club Africain, Tunisia), Hamzir Lahmar (Etoile, Tunisia), Youssef Msakni (Lekhwiya SC, Qatar).

Mshambuliaji Yassine Khenissi (ES de Tunis, Tunisia), Ahmed Akaichi (Al-Ittihad, Saudi Arabia), Saber Khalifa (Club Africain, Tunisia).

ZIMBABWE

Makipa: Donovan Bernard (How Mine), Takabva Mawaya (ZPC Kariba), Tatenda Mkuruva (Dynamos)
Nabeki: Teenage Hadebe, Lawrence Mhlanga (wote Chicken Inn), Onismor Bhasera (SuperSport Utd/Afrika Kusini), Bruce Kangwa (Azam/Tanzania), Oscar Machapa (V Club/Ivory Coast), Elisha Muroiwa (Dynamos), Costa Nhamoinesu (Sparta Prague/Jamhuri ya Czech), Hardlife Zvirekwi (CAPS Utd)
Viungo: Kudakwashe Mahachi, Danny Phiri (wote Golden Arrows/Afrika Kusini), Khama Billiat (Mamelodi Sundowns/Afrika Kusini), Willard Katsande (Kaizer Chiefs/Afrika Kusini, nahodha), Marvelous Nakamba (Vitesse Arnhem/Uholanzi)
Washambuliaji: Tinotenda Kadewere (Djurgardens/Sweden), Cuthbert Malajila (Wits/Afrika Kusini), Nyasha Mushekwi (Dalian Yifang/China), Knowledge Musona (Ostend/Ubelgiji), Tendai Ndoro (Orlando Pirates/Afrika Kusini), Evans Rusike (Maritzburg/Afrika Kusini), Mathew Rusike (CS Sfaxien/Tunisia)
Kundi C

IVORY COAST

Makipa: Sylvain Gbohouo (Mazembe, Kongo), Mande Sayouba (Stabaek, Norway), Ali Badra Sangare (Tanda, Ivory Coast).
Mabeki: Eric Bailly (Manchester United), Serge Aurier (Paris St-Germain, Ufaransa), Simon Deli (Slavia Prague, Czech), Wilfried Kanon (The Hague, Uholanzi), Lamine Kone (Sunderland), Adama Traore (Basel, Uswisi), Bagayoko Mamadou (Saint Truiden, Ubelgiji).
Viungo: Geoffrey Serey Die (Basel, Uswisi), Victorien Angban (Grenada, Hispania), Cheick Doukoure (Metz, Ufaransa), Franck Kessie (Bergamo, Italia), Yao Serge N'Guessan (Nancy, Ufaransa), Jean-Michael Seri (Nice, Ufaransa).
Washambuliaji: Wilfried Bony (Stoke City), Max Gradel (Bournemouth), Jonathan Kodjia (Aston Villa), Giovanni Sio (Rennes, Ufaransa), Salomon Kalou (Hertha Berlin, Ujerumani), Nicolas Pepe (Angers, Ufaransa), Wilfried Zaha (Crystal Palace).

MOROCCO

Makipa: Yassine El-Kharroubi (Lokomotiv Plovdiv, Bulgaria), Yassine Bounou (Girona, Hispania), Munir Kajoul Mohamedi (Numancia, Hispania)
Mabeki: Manuel da Costa (Olympiakos, Ugiriki), Mehdi Benatia (Juventus, Italia), Amine Attouchi (Wydad Casablanca), Fouad Chafik (Dijon, Ufaransa), Nabil Dirar (Monaco, Ufaransa), Hamza Mendyl (Lille, Ufaransa), Romain Saiss (Wolves)
Viungo: Mourir Obbadi (Lille, Ufaransa), Karim El-Ahmadi (Feyenoord, Uholanzi), Youssef Ait Bennasser (Nancy, Ufaransa), Mbarek Boussoufa (Al-Jazeera, UAE), Faycal Fajr (Deportivo La Coruna, Hispania), Mehdi Carcela (Grenada, Hispania), Omar El Kadouri (Napoli, Italia)
Washambuliaji: Rachid Alioui (Nimes, France), Youssef El-Arabi (Al-Lekhwiya, Qatar), Youssef Ennesyri (Malaga, Hispania), Khalid Boutaib (Racing Strasbourg, Ufransa), Aziz Bouhaddouz (St Pauli, Ujerumani).
Morocco bado haijamtanagza mchezaji atakayechukua nafasi ya Sofiane Boufal (Southampton), aliyejiondoa Januari 8.

TOGO

Makipa: Kossi Agassa (hana timu), Cedric Mensah (Le Mans, Ufaransa), Baba Tchagouni (Marmande, Ufaransa).
Mabeki: Serge Akakpo (Trabzonspor, Uturuki), Vincent Bossou (Young Africans, Tanzania), Dakonam Djene (St Truiden, Ubelgiji), Joseph Douhadji (River United, Nigeria), Maklibe Kouloun (Dyto Lome), Abdul Mamah Gaffar (Dacia, Moldovia), Sadat Ouro-Akoriko (Al Khaleej, Saudi Arabia), Hakim Ouro-Sama (Togo-Port).

Viungo: Lalawele Atakora (Helsingborg, Sweden), Franco Atchou (Dyto Lome), Floyd Ayite (Fulham), Razak Boukari (Chateauroux, Ufaransa), Mathieu Dossevi (Standard Liege, Ubelgiji), Henritse Eninful (Doxa Katakopias, Cyprus), Victor Nukafu Victor (Entente Deux), Alaixys Romao (Olympiakos, Ugiriki), Prince Segbefia (Goztepe, Uturuki).
Washambuliaji: Emmanuel Adebayor (hana timu), Komlan Agbegniadan (Wafa, Ghana), Ihlas Bebou (Fortuna Düsseldorf, Ujerumani), Serge Gakpe (Genoa, Italia), Kodjo Fo-Doh Laba (Renissance Berkane, Morocco).
Kundi D

MISRI
Makipa: Ahmed El-Shennawy (Zamalek, Misri) Essam El-Hadary (Wadi Degla, Misri), Sherif Ekramy (Al Ahly, Misri).

Mabeki: Ahmed Fathi (Al Ahly, Misri), Ahmed Elmohamady (Hull City), Mohamed Abdel-Shafy (Al-Ahli, Misri), Karim Hafez (Lens, Ufaransa), Ahmed Hegazy (Al Ahly, Misri), Saad Samir (Al Ahly, Misri), Ahmed Dweidar (Zamalek, Misri), Ali Gabr (Zamalek, Misri), Omar Gaber (Basel, Uswisi).
Viungo: Mohamed Elneny (Arsenal, England), Tarek Hamed (Zamalek, Misri), Ibrahim Salah (Zamalek, Misri), Abdallah El-Said (Al Ahly, Misri), Amr Warda (Panetolikos, Ugiriki), Ramadan Sobhi (Stoke City), Mahmoud Hassan (Royal Mouscron, Ubelgiji).
Washambuliaji: Ahmed Hassan (Braga, Ureno), Marwan Mohsen (Al Ahly, Misri), Mahmoud Abdel-Moneim (Al-Ittihad, Saudi Arabia), Mohamed Salah (AS Roma, Italia).
GHANA
Kipa: Razak Brimah (Cordoba/Hispania), Abdul-Fatau Dauda (Enyimba/Nigeria), Richard Ofori (Wa All Stars)

Mabeki: Harrison Afful (Columbus Crew/USA), Andy Yiadom (Barnsley), Baba Rahman (Schalke/Ujerumani), Frank Acheampong (Anderlecht/Ubelgiji), John Boye (Sivasspor/Uturuki), Jonathan Mensah (Columbus Crew/USA), Daniel Amartey (Leicester City), Edwin Gyimah (Orlando Pirates/Afrika Kusini)

Viungo: Emmanuel Agyemang-Badu (Udinese/Italia), Afriyie Acquah (Torino/Italia), Thomas Partey (Atletico Madrid/Hispania) Mubarak Wakaso (Panathinaikos/Ugiriki), Christian Atsu (Newcastle United), Ebenezer Ofori (AIK Stockholm/Sweden), Samuel Tetteh (Leifering/Austria)

Washambuliaji: Asamoah Gyan (Al Ahly/UAE), Jordan Ayew (Aston Villa), Andre Ayew (West Ham), Ebenezer Assifuah (Sion/Uswisi), Bernard Tekpetey (Schalke/Ujerumani)
MALI
Makipa: Soumaila Diakite (Stade Malien, Mali), Djigui Diarra (Stade Malien, Mali), Oumar Sissoko (Orleans, Ufaransa).
Mabeki: Ousmane Coulibaly (Panathinaikos, Greece), Hamari Traore (Stade de Reims, France), Molla Wague (Udinese, Italia), Salif Coulibaly (TP Mazembe, Congo DR), Mohamed Oumar Konate (RS Berkane, Morocco), Mahamadou N'Diaye (Troyes, Ufaransa), Youssouf Kone (Lille, Ufaransa), Charles Traore (Troyes, Ufaransa).

Viungo: Yves Bissouma (Lille, Ufaransa), Mamoutou Ndiaye (Antwaerp, Ubelgiji), Lassana Coulibaly (Bastia, Ufaransa), Yacouba Sylla (Montpellier, Ufaransa), Samba Sow (Kayseryspor, Uturuki), Adama Traore (Monaco, Ufaransa), Sambou Yatabare (Werder Bremen, Ujerumani).
Washambuliaji: Moussa Doumbia (Rostov, Russia), Moussa Marega (Guimares, Ureno), Kalifa Coulibaly (La Gantoise, Belgium), Moustapha Yatabare (Kardemir Karabukspor, Turkey), Bakary Sako (Crystal Palace).
Uganda
Makipa: Robert Odongkara (Saint George, Ethiopia), Magoola Salim Omar (El Merriekh, Sudan), Denis Onyango (Mamelodi Sundowns, Afrika Kusini).
Mabeki: Azira Michael (Colorado Rapids, Marekani), Awany Timothy Dennis (KCCA, Uganda), Joseph Ochaya (KCCA, Uganda), Geoffrey Kizito (Than Quang Ninh, Vietnam), Murushid Juuko (Simba, Tanzania), Isaac Isinde (hana timu), Denis Iguma (Al Ahed, Lebanon), Nico Wadada Wakiro (Vipers, Uganda).
Viungo: Tony Mawejje (Thotur, Iceland), Sentamu Junior Yunus (Ilves, Finland), Khalid Aucho (Baroka, Afrika Kusini), Batambuze Shafik (Tusker, Kenya), Muhammad Shaban (Onduparaka, Uganda), Moses Oloya (Hanoi T and T, Vietnam), Godfrey Walusimbi (Gor Mahia, Kenya), Hassan Mawanda Wasswa (Nijmeh, Lebanon).
Washambuliaji: Geofrey Sserunkuma (KCCA, Uganda), Luwagga William Kizito (Rio Ave, Ureno), Geoffrey Massa (Baroka, Afrika Kusini), Faruku Miya (Standard Liege, Ubelgiji).





































No comments:

Post a Comment