Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, December 16, 2016

ZAHORO PAZI AMTUMIA UJUMBE RAIS WA TFF, JAMAL MALINZI




MSHAMBULIAJI Zahoro Pazi aliyesajiliwa Mbeya City amemtumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS) Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jamal Malinzi akimuomba kumsaidia ili apate ITC yake inayoshikiliwa na timu ya FC Lupopo ya DR Congo.
Endapo Pazi atashindwa kupata ITC hiyo itakuwa vigumu kucheza mechi za Ligi Kuu Bara ambapo kesho Jumamosi City wanaikaribisha Kagera Sugar na huenda akakosa mechi hiyo.
Katika ujumbe huo, Pazi alikwenda mbali zaidi kwa kumueleza Malinzi kuwa suala lake linafahamika huku akidai kuwa mchezo mzima ulichezwa na Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura aliyetoa kibali chake kwenda Lupopo na sasa TFF haimpi ushirikiano wa kupata kibali hicho.

No comments:

Post a Comment