Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, December 13, 2016

UEFA EUROPA LIGI-DROO YA RAUNDI YA MTOANO: MAN UNITED vs ST-ETIENNE, ASTRA GIURGIU vs GENK


DROO ya Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya UEFA EUROPA LIGI imefanyika Leo huko Nyon, Uswisi na Manchester United kupangwa na St-Etienne ya France.
St-Etienne ni Timu ambayo Kaka wa Kiungo wa Man United, Paul Pogba, anachezea ambae huitwa Florentin.
Hivi sasa St-Etienne wanakamata Nafasi ya 8 kwenye Ligi 1 huko France.
Nayo Klabu ya Straika wa Tanzania, Mbwana Samatta, Genk ya Belgium imepangiwa Astra Giurgiu ya Romania.
Timu nyingine ya England ambayo iko EUROPA Ligi, Tottenham, itacheza na Klabu ya Belgium Gent.
Mechi hizo za Raundi ya Mtoano ya Timu 32 zitachezwa Alhamisi Februari 16 na Marudiano ni Februari 23.

JE WAJUA?
-Manchester United wamepoteza Mechi 1 tu kati ya 16 walizocheza mwisho na Klabu za France Wakishinda 9 na Sare 6.
Straika wa Man United United Zlatan Ibrahimovic ambae alitokea Paris St-Germain ya France amefunga Bao 14 katika Mechi 13 dhidi ya St Etienne, ikiwa ni idadi kubwa kupita Timu yeyote huko France.


DROO KAMILI:

Athletic Bilbao vs Apoel Nicosia
Legia Warsaw vs Ajax
Anderlecht vs Zenit St Petersburg
Astra Giurgiu vs Genk
Manchester United vs Saint-Etienne
Villarreal vs Roma
Ludogorets vs FC Copenhagen
Celta Vigo vs Shakhtar Donetsk
Olympiakos vs Osmanlispor
Gent vs Tottenham Hotspur
Rostov vs Sparta Prague
Krasnodar vs Fenerbahce
Borussia Monchengladbach vs Fiorentina
AZ Alkmaar vs Lyon
Hapoel Beer Sheva vs Besiktas
PAOK vs Schalke

UEFA EUROPA LIGI
Tarehe Muhimu:

16/02/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 32, Mechi za Kwanza
23/02/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 32, Marudiano
09/03/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Mechi za Kwanza
16/03/17: Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Marudiano
13/04/17: Robo Fainali, Mechi za Kwanza

No comments:

Post a Comment