Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, October 14, 2016

TFF KUBADILI UBUNIFU WA JEZI ZA TIMU ZA TAIFA


Taifa Stars of Tanzania
Image result for taifa stars images
SHIRIKISHO la soka nchini Tanzania (TFF) limesema mchakato wa ubunifu wa jezi za timu Taifa umeachwa kwa wabunifu wa mavazi pamoja na wadau wengine.
Akizungumza na gazeti hili Ofisa habari wa TFF Alfred Lucas amesema mpango wa ubunifu wa jezi mpya za timu za Taifa, umeibuliwa tena kutokana na mikakati iliyowekwa na uongozi uliopo madarakani.
"Kila inapopita miaka miwili tuhakikisha kila ni lazima timu za Taifa ziwe katika mtazamo tofauti kimavazi", alisema Lucas.
Lucas amesema suala hilo wamemaua kulifanya kuwa wazi kwa kila mdau kushiriki kikamilifu ili kupata muundo na muonekano mzuri wa jezi ambazo zitaanza kutumika mwaka ujao.
Muundo wa ubunifu wa jezi zinazotumika kwa sasa na timu za Taifa ulibadilishwa na uongozi wa Rais Jamal Malinzi jambo ambalo lilizua malalamiko kwa wadau, wakisema rangi zake hazina mvuto na hazileti utaifa.
Timu za Taifa zinatumia jezi za rangi nyeupe juu na chini zikiwa na kola ya kijani ugenini na nyumbani zinavaa jezi za rangi ya bluu juu na chini shingoni zikiwa na kola ya kijani.

No comments:

Post a Comment