Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, September 9, 2016

KILIMANJARO QUEENS YAICHAPA BURUNDI MABAO 3-0

 

Kikosi cha Timu ya Mpira wa Miguu ya Taifa ya wanawake wa Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens kilichoanza leo kwenye mchezo wa Kimataifa wa Kirafiki ulichezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba Bukoba Mjini leo na kuibuka na ushindi wa bao 3-0.
Na Faustine Ruta, Bukoba
Bao zote za  Kilimanjaro Queens zilifungwa kipindi cha kwanza, Bao la kwanza  limefungwa na Asha Rashid dakika ya 22, Bao la pili lilifungwa na Mwanahamisi Omary dakika ya 30 huku

Bao la tatu lilikuwa la kujifunga wao wenyewe baada  ya mabeki wa Burundi kujichanganya na mchezaji Niyonkulu Saidauze kwenye harakati za kutaka kuokoa mpira kwenye eneo hatari dakika ya 33. Hadi dakika 90 zinamalizika Kilimanjaro Queens ndio walikuwa wababe  kwa kutoka na ushindi wa bao 3-0. Mchezo huo wa kirafiki wa Kimataifa uliokuwa ni moja ya Timu zote mbili kujiandaa  na Michezo ya CECAFA Nchini Uganda. Na Kesho Timu zote mbili zinaelekea jijini Jinja, Nchini Uganda.
Kikosi cha Timu  ya Mpira wa Miguu ya Taifa ya wanawake Burundi kilichoanza leo dhidi ya Kilimanjaro Queens.Timu ya Wanawake wa Tanzania Bara maarufu kwa jina la Kilimanjaro Queens wakiomba kabla ya Mechi kuanza.
Burundi wakipanga mbinu na kuwabana Kilimanjaro Queens punde kabla ya kipute kuanza
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu akisalimiana na waamuzi


No comments:

Post a Comment