MMILIKI
wa Klabu ya Chelsea Roman Abramovich amewaambia Wachezaji wa Klabu hiyo
kuwa Antonio Conte ndie atakuwa Meneja mpya Msimu ujao kwa mujibu wa
ripoti toka Italy.
Conte, mwenye Miaka 46, ni Meneja wa Timu ya Taifa ya Italy na Mkataba wake unamalizika mara baada ya kwisha kwa EURO 2016 mapema Mwezi Julai.
Kabla kushika wadhifa Timu ya Taifa ya Italy, Conte alikuwa Kocha Mkuu wa Juventus kuanzia 2011 hadi 2014 na kuiwezesha kutwaa Mataji Matatu ya Ubingwa wa Italy mfululizo.
Kwa mujibu wa Jarida la Italy, Corriere dello Sport, Abramovich amewahakikishia Wachezaji wa Chelsea kuwa Conte ndie Meneja mpya wakati alipokutana na Kikosi chote kwenye Kituo cha Mazoezi cha Timu hiyo huko Cobham Mjini London.
Hivi sasa Chelsea wana Meneja wa muda Guus Hiddink ambae Mkataba wake unamalizika mwishoni mwa Msimu baada ya kuteuliwa kuchukua nafasi ya Jose Mourinho alieondolewa Mwezi Desemba.
Tangu wakati huo, Hiddink ameisimamisha wima Chelsea na kupanda kwenye Ligi Kuu England hadi Nafasi ya 10 toka Nafasi za mkiani Mwezi Desemba ikiwa sasa Pointi 8 tu nyuma ya Timu ya 4 kwenye Ligi.
Conte, mwenye Miaka 46, ni Meneja wa Timu ya Taifa ya Italy na Mkataba wake unamalizika mara baada ya kwisha kwa EURO 2016 mapema Mwezi Julai.
Kabla kushika wadhifa Timu ya Taifa ya Italy, Conte alikuwa Kocha Mkuu wa Juventus kuanzia 2011 hadi 2014 na kuiwezesha kutwaa Mataji Matatu ya Ubingwa wa Italy mfululizo.
Kwa mujibu wa Jarida la Italy, Corriere dello Sport, Abramovich amewahakikishia Wachezaji wa Chelsea kuwa Conte ndie Meneja mpya wakati alipokutana na Kikosi chote kwenye Kituo cha Mazoezi cha Timu hiyo huko Cobham Mjini London.
Hivi sasa Chelsea wana Meneja wa muda Guus Hiddink ambae Mkataba wake unamalizika mwishoni mwa Msimu baada ya kuteuliwa kuchukua nafasi ya Jose Mourinho alieondolewa Mwezi Desemba.
Tangu wakati huo, Hiddink ameisimamisha wima Chelsea na kupanda kwenye Ligi Kuu England hadi Nafasi ya 10 toka Nafasi za mkiani Mwezi Desemba ikiwa sasa Pointi 8 tu nyuma ya Timu ya 4 kwenye Ligi.
No comments:
Post a Comment