Waziri Nape akiongea na wandishi wa habari leo, kulia ni Mwenyekiti wa BMT, Dioniz Malinzi na kushoto ni Katibu wa BMT, Henry Lihaya ambaye aneondolewa na Nape |
WAZIRI wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo,Nape Nnauye ametengua
uteuzi wa Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo Tanzani, Henry Lihaya baada ya kushindwa kutekeleza
wajibu wake.
Nnauye alitengua
uteuzi huo jana alipofanya ziara katika ofisi za BMT kuona miundo mbinu ya
ofisi hizo na kujua changamoto zinazowakabili.
“Baraza likirekebishwa vyama vya michezo navyo vinatekeleza majukumu yao na kuleta chachu na maendeleo katika michezo,”alisema Nnauye.
Pia alisema miaka saba ambayo Lihaya amekuwa Katibu Mtendaji wa Baraza imetosha kwani hakuna mabadiliko yoyote aliyoyafanya katika sekta ya michezo tangu alipoteuliwa mwaka 2009.
Kutokana na utenguzi huo Nnauye amemtaka Mwenyekiti wa BMT Dionis Malinzi kupendekeza jina la Katibu Mtendaji mpya wa BMT kwa mujibu wa sheria ya BMT kifungu cha 5(1).
Vilevile Nnauye amemtaka Malinzi kuteua Katibu Mtendaji ambaye atakuwa ni mchapa kazi na mwenye mipango ambayo itaibadilisha BMT na kuleta chachu katika michezo nchini.
Nnauye amemuagiza Katibu
Mkuu wa wizara ya habari, utamaduni Sanaa na Michezo kumpangia Lihaya kazi
nyingine wizarani.
No comments:
Post a Comment