Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, January 2, 2016

Gerrard:2016 mwaka wangu wa mwisho kucheza soka

football-gerrard-steven_3304393

Mchezaji wa zamani wa Liverpool ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya LA Galaxy ya nchini Marekani, Steven Gerrard amesema anapenda kustaafu kucheza soka mwaka huu na kufanya kazi nyingine.
Gerrard ambaye ambaye aliondoka Liverpool mwaka uliopita na kwenda kucheza Ligi ya Marekani MLS ambayo kwa sasa imemalizika ameliambia gazeti la Telegraph kuwa hana uhakika kwa asilimia zote kama utakuwa mwaka wake wa mwisho lakini anapendelea iwe hivyo.
“Sina asilimia 100 lakini nafikiri utakuwa mwaka wangu wa mwisho wa kuwa kama mchezaji,” alisema Gerrard.
Baada ya kuelezea mipango yake ya kutaka kustafu kucheza mpira mwaka huu, Gerrard amezungumzia mipango yake baada ya kustaafu na kusema kuwa anapendelea kuja kuwa kocha na huku akijilaumu kwa kutokutumia muda wake vizuri aliokuwa nao na badala yake muda mwingi kuwa akitumikia katika timu ya taifa ya Uingereza.
“Kiuhakika naweza kuanza kupatikana mwezi Novemba au Disemba, 2016, kila mtu wa soka duniani atajua kuwa kwa uhakika napatikana na nina matumaini 75% nitakwenda katika mafunzo ya ukocha,
“Nilikataa kuanza mafunzo ya ukocha nikiwa na miaka 21 au 22, muda wote nilipoteza nikitumikia timu ya taifa katika hoteli kama mchezaji wa timu hiyo hata nilipokuwa sina kazi ya kufanya nilikuwa naangalia tu ofisi na kuangalia muziki wa bendi, natamani kama ningekuwa na CBA [leseni ya ukocha] na sasa ningekuwa nafanya majaribio ya leseni yangu.

No comments:

Post a Comment