Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, December 22, 2015

THEO WALCOTT NA GIROUD WAIPA USHINDI ARSENAL IKIIFUNGA MANCHESTER CITY 2-1

LIGI KUU ENGLAND Usiku huu imemalizia Raundi ya Mechi zake za 17 kuelekea zile Mechi mfululizo za mwishoni mwa Mwaka kwa mtanange uliochezwa Emirates Jijini London wa Timu ambazo hasa ndizo zinapewa nafasi za kutwaa Ubingwa kwa Arsenal kuifunga Manchester City Bao 2-1.
Dakika 90 zimekamili 2-1 Arsenal waibuka kidedea...2-0

Ushindi huu umewabakisha Arsenal Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Leicester City wakati City wakiwa Nafasi ya 3 Pointi 4 nyuma ya Arsenal wakifuatiwa na Spurs na Man United ambazo ziko Pointi 3 nyuma huku kila Timu ikiwa imecheza Mechi 17.
Arsenal walitangulia kufunga katika Dakika ya 33 baada ya pasi ya Mesut Ozil kumkuta Theo Walcott Winga ya kushoto na kisha kumhadaa Fulbeki wa City, Bacary Sagna, na kuachia kigongo cha Mguu wa kushoto kilichomshinda Kipa Joe Hart na kutinga.

Dakika ya 45 Olivier Giroud aliipa Bao la Pili Arsenal baada ya kutengenezewa na Mesut Ozil
Hadi Haftaimu Arsenal 2 Man City 0.
Dakika ya 82 City walirudi kwenye Gemu na kuwa 2-1 kwa Goli la Yaya Toure kufuatia kupasiana vyema na yeye kumalizia vizuri kwa shuti la kupinda lililomhadaa Kipa Petr Cesc.
Kuanzia hapo City walikuja juu lakini Arsenal walisimama imara kulinda uongozi wao na kuibuka Washindi.

1-0Theo Walcott akipongezwa baada ya kufunga bao la kwanza.VIKOSI:
Arsenal starting XI:
Cech, Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Ramsey, Flamini, Walcott, Ozil, Campbell, Giroud
Arsenal subs: Gibbs, Gabriel, Ospina, Oxlade-Chamberlain, Chambers, Iwobi, Reine-Adelaide
Manchester City starting XI: Hart, Sagna, Otamendi, Mangala, Kolarov, Fernandinho, Toure, Delph, De Bruyne, Silva, Aguero
Man City subs: Sterling, Caballero, Bony, Jesus Navas, Clichy, Demichelis, Iheanacho

Hii ndiyo mechi ya mwisho ya Ligi Kuu England kabla ya sikukuu ya Krismasi. Arsenal wanakuwa wenyeji wa Manchester City kwenye Uwanja wa Emirates jijini London. Mechi inasubiriwa kwa hamu kubwa, wengi wanaonekana kuipa nafasi Arsenal ingawa soka halina mwenyewe. Mechi tano zilizopita kwa kila timu, inaonekana Arsenal imeshinda mara nne na sare moja. Upande wa City, nao wameshinda mechi nne, wamepoteza moja. Si mechi ya mzaha wala hakuna anayeweza kuwa na uhakika kwa kuwa uwezo kwa timu hizo unaonekana kulingana kabisa na ndiyo zimekuwa zikibadilishana kiti cha kileleni

No comments:

Post a Comment