Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, December 19, 2015

TAMBWE APIGA HATTRICK YANGA IKIIFUNGA STAND 4-0, SIMBA YATOKA SARE NA TOTO





YANGA leo imeendelea kujiweka vizuri katika harakati zake za kutetea ubingwa wa Ligi Kuu baada ya kuichapa Stand United mabao 4-0 katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Matokeo hayo yanaifanya Yanga iendelee kukaa kileleni ikiwa na pointi 30 huku Azam iliyo nafasi ya pili ikiwa na pointi 26 lakini ikiwa nyuma mechi mbili. Azam leo inatarajiwa kucheza na Majimaji Songea.

Mechi hiyo ilianza kwa timu kushambuliana kwa zamu lakini iliichukua Yanga dakika 18 kuandika bao la kuongoza lililofungwa na Amisi Tambwe baada ya kuunganisha pasi nzuri ya Thaban Kamusoko.

Kuingia kwa bao hilo ni kama kuliiamsha Stand ambapo dakika ya 28 mshambuliaji wake Elius Maguli alifurukuta lakini nafasi ya wazi ya kufunga aliyoipata alishindwa kuitumia.

Tambwe aliwainua tena vitini mashabiki wa Yanga baada ya kuongeza bao la pili katika dakika ya 36 kwa kuunganisha pasi ya Juma Abdul.

Dakika moja kabla ya kwenda mapumziko, Tambwe aliandika bao la tatu  safari hii akigongeana vizuri na Donald Ngoma.

Dakika ya 62 Kamusoko aliifungia Yanga bao la nne pasi ikiwa na Abdul tena. Stand katika mechi ya jana ilionekana kuzidiwa kuanzia dakika ya 20 za kipindi cha kwanza. Maguli na Haruna Chanongo walikosa mabao katika dakika ya 40 na 42.

Kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, Simba ilitoka sare ya bao 1-1 na wenyeji Toto Africans.
  
Daniel Lyanga ndiye aliifungia Simba bao la kuongoza katika dakika ya 22 kwa shuti kali akiwa nje ya 18. Everisti Benard aliifungia Toto bao la kusawazisha baada ya beki Hassan Isihaka kushindwa kuruka juu na kupiga kichwa, mpira ukamkuta mfungaji akaukwamisha wavuni.


No comments:

Post a Comment