
Kabla Ligi Kuu England kusimama, Chelsea ilifungwa na Stoke City na hicho kulikuwa kipigo chao cha 3 mfululizo kwenye Ligi kilichowabwaga hadi Nafasi ya 16 wakiwa Pointi 1 nyuma ya wapinzani wao wa Jumamosi Norwich City na Pointi 3 juu ya zile Timu 3 za mkiani.

Kwa Wachambuzi wengi huko England tatizo la Chelsea ni kuwa wengi wa Wachezaji wao wanacheza chini ya kiwango tofauti na Msimu uliopita walipotwaa Ubingwa.


Pengine habari njema kwa Mourinho katika wakati wake mgumu ni kupona kwa Kipa wake Nambari Wani Thibaut Courtois ambae amerejea mazoezini lakini Asmir Begovic ndie ataeikabili Norwich.
Norwich, licha ya kuwa Pointi 1 juu ya Chelsea, walitoka kwenye wimbi la vipigo vya Mechi 4 za Ligi na kushinda Mechi yao ya mwisho walipoibwaga Swansea City.
No comments:
Post a Comment