KOZI
ya waamuzi wa mpira wa miguu
watakaochezesha mechi za Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza 2015/2016,
inatarajiwa kutafanyika jijini Dar es salaam kuanzia Agosti 21 -24.
Akizungumza
na wandishi wa habari Afisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) , Baraka Kizuguto, alisema shirikisho
kozi ya waamuzi watakaochezesha
mechi za Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza msimu wa 2014/2015 wenye umri wa
miaka 21 – 45 kwa wanawake na miaka 23 – 45 kwa wanaume.
“Waamuzi
wote wanatakiwa kuripoti Agosti 21 katika ofisi za TFF zilizopo Karume Ilala
Dar es salaam na wawasilishe vyeti halisi vya kuzaliwa na nakala zake”, alisema
Kizuguto
Pamoja
na cheti cha kuzaliwa kwa kila mwamuzi ni lazima alete kadi ya kupigia kura au
passport ya kusafiria kwa ajili ya uthibitisho wa umri wake.
Washiriki
wa kozi watafanya mitihani ya kupima afya, utimamu wa mwili na sheria za mpira
wa miguu Trivia (kuandika), mikanda ya video za sheria za soka na uchambuzi wa
mechi.
Waamuzi
watakaofaulu watashindanishwa kupata waamuzi 40 na waamuzi wasaidizi 70
watakaochezesha Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza kwa msimu wa 2015/2016.
Baada
ya kozi ya waamuzi kutakuwa na kozi ya makamisaa wa Ligi Kuu na Ligi Daraja la
Kwanza ambayo itafanyika kuanzia Agosti 24-25 na wanatakiwa kuripoti Agosti 23saa
10:00 alasiri uwanja wa Taifa.
Makamisaa
watafanya mtihani wa sheria za mpira wa miguu, na kupima mwamuzi
anapochezesha na wale watakaofaulu ndiyo
watakaopangwa kusimamia michezo hiyo.
No comments:
Post a Comment