Baadhi ya wachezaji waliohudhuria mazishi ya baba yake Haruna Moshi |
Shirikisho
la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limetuma salamu za rambi rambi kwa familia ya
Moshi Shaban, kufutia kifo cha Moshi kilichotokea jana jijini Dar s salaam na mazishi yamefanyika leo
Katika
salamu zake za rambirambi kwa familia ya marehemu Moshi, TFF imewapa pole
wafiwa, ndugu jamaa na marafiki na kusema wako pamoja katika kipindi hiki cha
maombelezo na kuomba mwenyezi Mungu awajilie nguvu wafiwa
Marehemu
Moshi Shaban ni baba wa wachezaji waliowahi kuichezea timu ya Taifa ya
Tanzania, Haruna Moshi “Boban) na Iddy Moshi (Mnyamwezi).
No comments:
Post a Comment