
Liverpool wameafikiana dili ya kunsaini
Kijana wa Miaka 22 anaecheza kama Straika wa Burnley iliyoporomoka
Daraja kutoka Ligi Kuu England licha ya Klabu hiyo kuigomea ofa ya
Liverpool.
Danny Ings, anaechezea Timu ya Taifa ya
England ya U-21, anamaliza Mkataba wake na Burnley mwishoni mwa Mwezi
huu lakini kutokana na umri wake mdogo Kanuni zinaitaka Liverpool
kuilipa fidia Burnley. Liverpool wanatarajia kulipa fidia ya kati ya Pauni Milioni 5 hadi 6 lakini ikiwa Burnley watagoma basi suala hilo litaenda kwenye Jopo litakaloamua idadi inayofaa.
Wakati Burnley imesema itaendelea maongezi na Liverpool, Vigogo hao wa England wametangaza watamsaini Ings Julai 1 baada ya kukubaliana malupulupu yake binafsi na ikiwa Mchezaji huyo atafuzu upimwaji afya yake.


No comments:
Post a Comment