Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, June 25, 2015

KIPA HUGO WA SPURS NJIANI KUTUA OLD TRAFFORD

Zipo ripoti nzito toka England zinazodai Meneja wa Manchester United Louis van Gaal na Kipa wa Tottenham Hugo Lloris wamefikia muafaka na Kipa huyo wa Kimataifa wa France ambae ameshakubaliana kuhusu maslahi yake binafsi huko Old Trafford.
Huku kukiwa na mipango ya chini chini ya Kipa Nambari Wani David de Gea kurudi kwao Spain kuidakia Real Madrid, kumchukua Hugo Lloris kunaelekea kuziba pengo hilo.Kwa mujibu wa chanzo cha habari hizi, Gazeti linaloheshimika huko France L'Equipe, kilichobaki sasa ni mazungumzo ya kukubaliana Ada ya Uhamisho na Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy.
L'Equipe imedai Levy amemhakikishia Lloris kuwa Klabu yeyote itakayotoa Ofa ya Pauni Milioni 18 kwenda juu basi atamruhusu kuhama White Hart Lane.Lloris, mwenye Miaka 28, alijiunga na Tottenham Mwaka 2012 akitokea Lyon ya France kwa Dau la Pauni Milioni 11.4.
Hata hivyo, Levy anasifika mno kwa ugumu wa kutoa Wachezaji wake Nyota na kama akiwaruhusu basi Dau lao huwa sio masihara.


Juan Mata

No comments:

Post a Comment