Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, June 25, 2015

WENYEJI CHILE NUSU WASONGA FAINALI, WAKIWABWAGA URUGUAY BAO 1-0, COPA AMERICA


Wakicheza kwao Estadio Nacional de Chile, Santiago, Chile wameifunga Mtu 9 Uruguay Bao 1-0 na kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Marekani ya Kusini, COPA AMERICA.
Bao hilo la Chile lilifungwa na Mauricio Isla katika Dakika ya 81 wakati Uruguay, Mabingwa Watetezi, wakicheza Mtu 10 baada ya Edinson Cavani kutolewa kwa Kadi Nyekundu katika Dakika ya 63 kufuatia Kadi ya Njano ya PIli.Cavani alipewa Kadi ya Njano ya kwanza katika Dakika ya 29.
Katika Dakika ya 88 Uruguayl ilibaki Mtu 9 baada Jorge Fucile kupewa Kadi Nyekundu baada kujizolea Kadi za Njano mbili.
Kwenye Nusu Fainali, Chile watacheza na Mshindi kati ya Bolivia na Peru wanaocheza Usiku huu.
RATIBA
ROBO FAINALI
Jumatano Juni 24

Chile 1 vs Uruguay 0
Alhamisi Juni 25
Bolivia vs Peru (Saa 8:30Usiku)
Ijumaa Juni 26
Argentina vs Colombia (Saa 8:30Usiku)
Jumamosi Juni 27
Brazil vs Paraguay (Saa 6:30 Usiku)
NUSU FAINALI
Jumatatu Juni 29

Chile vs Bolivia/Peru (Saa 8:30 Usiku)
Jumanne Juni 30
Argentina/Colombia vs Brazil/Paraguay (Saa 8:30 Usiku)

MSHINDI WA 3
Ijumaa Julai 3

(Saa 8 na Nusu Usiku)
FAINALI
Jumamosi Julai 4

(Saa 5 Usiku)

No comments:

Post a Comment