Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, May 2, 2015

DANIEL STURRIDGE AENDA MAREKANI KWA MATIBABU


Mshambuliaji Liverpool Dan Sturridge huenda akafanyiwa upasuaji ili kutibu tatizo la nyonga linalomsumbua.
Mshambuliaji huyu ameelekea nchi Marekani kwenda kuonana na madaktari Peter Asnis ili kujua kama anahitaji kufanyiwa upasuaji kutibu tatizo lake.
Majeruhi yamekua yakimuandama mshambuliaji huyu katika msimu huu na kushindwa kuonyesha cheche zake za kuzifumania nyavu.
Aliumia mguu mwezi September wakati wa michezo ya kimataifa na kabla ya kuumia misuli akiwa mazoezini.

Akapata maumivu tena mwezi November , yaliyomuweka nje ya dimba mpaka January 31 ambapo alirudi uwanjani kucheza mchezo dhidi ya West Ham na kufunga mabao mawili.
Sturridge alijiunga na Liverpool kwa usajili wa kiasi cha pauni milioni 12 mwezi January mwaka 2013 na amefunga mabao 24 katika michezo yote aliyoichezea timu hiyo.
The Liverpool and England striker spent time in Boston in December, here pictured at the Red Sox gym

No comments:

Post a Comment