Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, March 8, 2015

FABIAN DELPH NA SINCLAIR WAIPA USHINDI VILLA NA KUSONGA HATUA YA NUSU FAINALI FA CUP

Aston Villa leo wameifunga Timu ya West Bromwich Albion bao 2-0. Bao za Villa zilifungwa na Fabian Delph dakika ya 51 na lile la dakika ya mwishoni la Scott Sinclair dakika ya 85 alipowachanganya mabeki wa West Brom Albion kwa kuwapiga chenga na kuachia shuti na kumfunga kipa huyo wa West Brom Albion.
Kocha Tim Sherwood akishangilia.
Aston Villa imetinga Nusu Fainali ya FA CUP baada ya Jana kuwachapa West Bromwich Albion Bao 2-0 Uwanjani Villa Park.
Bao za Villa kwenye Dabi hii ya Midlands zilifungwa Kipindi cha Pili na Fabian Delph na Scott Sinclair.

WBA walimaliza Mechi hii wakwa Mtu 10 baada ya Claudio Yacob kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu kufuatia Kadi za Njano mbili.
Mechi hii ilishuhudia Mashabiki wakivamia Uwanja kabla Filimbi ya mwisho kupigwa na ililazimika watelowe ili Mechi iendelee.
Katika Mechi nyingine ya Robo Fainali, Bradford na Reading zilitoka 0-0.

Hii Leo huko Anfield, Liverpool watacheza na Blackburn Rovers katika Robo Fainali nyingine ya FA CUP, Raundi ambayo itamalizika Jumatatu Usiku huko Old Trafford wakati Man United watakapocheza na Mabingwa Watetezi Arsenal.
Fabian Delph akishangilia bao lake baada ya kufanya 1-0 dhidi ya West Brom AlbionWachezaji wa Villa wakipongezwa na Mashabiki wao baada ya kuipiga bao 22-0 na kutinga Nusu Fainali
VIKOSI:
Aston Villa: Given, Bacuna, Okore, Clark, Lowton, Cleverley, Westwood, Delph, N'Zogbia, Agbonlahor, Sinclair.
Akiba: Guzan, Weimann, Sanchez, Gil, Kinsella, Calder, Grealish.

West Brom: Myhill, McAuley, Dawson, Olsson, Lescott, Yacob, Morrison, Berahino, Gardner, Brunt, Ideye.
Akiba: Foster, Wisdom, Baird, Pocognoli, McManaman, Mulumbu, Sessegnon.
Refa: Anthony Taylor

No comments:

Post a Comment