Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, March 8, 2015

RYAN GIGGS: HATUJATOFAUTIANA WALA KUKOSANA NA VAN GAAL

Naibu mkufunzi katika timu ya Manchester United Ryan Giggs amepinga madai ya mkwaruzano kati yake na mkufunzi wa kilabu hiyo Louis Van Gaal.
Uvumi wa wasiwasi kati ya makocha hao wawili ulizuka baada ya Giggs kukataa kusherehekea bao la ushindi la Ashley Young siku ya jumatano.
Aliyekuwa mchezaji mwenza katika kilabu hiyo Paul Scholes alisema kwamba Giggs amechoka kuwa mkufunzi chini Ya Louis Van Gaal kwa miaka mitatu ijayo.
Lakini Giggs amesema kuwa wawili hao wana ushirikiano mzuri kati yao na kwamba anafurahia kazi yake chini ya mkufunzi Van Gaal.

No comments:

Post a Comment