Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, January 24, 2015

RATIBA LIGI KUU VODACOM WIKIENDI HII, LEO NI POLISI MORO vs YANGA, JUMAPILI AZAM FC v SIMBA


Ligi Kuu Vodacom, Leo ipo dimbani kwa Mechi moja tu huko Uwanja wa Jamhuri Mini Morogoro na Jumapili zipo Mechi 6 na Bigi Mechi ni Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kati ya Mabingwa Azam FC na Simba.
Mechi nyingine za Jumapili ni pamoja na ile ya Kagera Sugar na Ndanda FC ambayo itachezwa Uwanja wa CCM Kirumba, Jijini Mwanza kutokana na Kairaba Stadium ya huko Bikoba kufanyiwa ukarabati.
Hadi sasa VPL inaongozwa na Azam FC wenye Pointi 20 kwa Mechi 10 wakifuata Mtibwa Sugar wenye Pointi 17 kwa Mechi 9 na kisha wapo JKT Ruvu wenye Pointi 17 kwa Mechi 11 na kufuata Yanga wenye Pointi 15 kwa Mechi 9.

RATIBA:
Jumamosi Januari 24

Polisi Morogoro v Yanga
 

Jumapili Januari 25
Azam FC vs Simba
Kagera Sugar vs Ndanda FC (CCM Kirumba, Mwanza)
Stand United vs Coastal Union
Mbeya City vs Tanzania Prisons
Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar
JKT Ruvu vs Mgambo JKT

No comments:

Post a Comment