Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, November 16, 2014

MAJERUHI OLD TRAFFORD WAFIKIA 10, KIPA DE GEA ATEGUKA KIDOLE HUKO SPAIN

Kipa wa Manchester United David De Gea amezidi kuleta kizaazaa Klabuni kwake baada ya kujiunga na Listi ndefu ya Majeruhi alipoteguka Kidole kidogo cha Mkononi akiwa Mazoezini na Spain.

Shirikisho la Soka la Spain, RFEF, limethibitisha kuumia kwa De Gea, mwenye Miaka 24, na kusema ataikosa Mechi ya Leo hii YA Kundi C la EURO 2016 kati ya Spain na Belarus itakayochezwa huko Huelva Nchini Spain.

Hata hivyo, De Gea bado yupo chini ya uchunguzi wa Jopo la Madktari wa Spain ambao watatoa uamuzi kama Kipa huyo arudishwe Klabuni kwake Man United au la.

Majuzi, Kiungo wa Man United, Michael Carrick, nae alipata maumivu ya Nyonga akiwa na Timu ya Taifa ya England na kuondoka Kambini kurudi Manchester.

No comments:

Post a Comment