Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, September 12, 2014

Uhuru Selemani: Kwangu mimi Patrick Phiri ni kama mzazi wangu sasa nacheza mpira kwa amani


Winga wa Simba Uhuru Selemani amesema kwasasa anajisikia faraja na kujiona ni mwenye amani zaidi tangu kurejea kwa kocha Mzambia Patrick Phiri.
Akiongea na Rockersports Uhuru amesema Phiri kwake ni kama mzazi ambaye amekuwa akimpa nasaha mara kwa mara na kumrejesha mchezoni kisaikolojia jambo ambalo anamini litamfanya sasa kucheza soka kwa kiwango chake tofauti na misimu miwili iliyopita.
Akiongea kwa masikitiko Uhuru amesema ilifika wakati alikata tamaa kabisa ya kucheza mpira kwa kiwango cha juu kutokana na kukosa nafasi katika kikosi cha Simba na hata thamani yake kushuka ndani ya wekundu hao wa Msimbazi.
Amesema tangu kurejea kwa Phiri mambo yamebadilika kwakuwa kocha huyo ameanza kumuamini tena na sasa anacheza mpira wake ule ule wa zamani.
"nashukuru mungu Phiri ni kama mzazi kwangu ananishauri mambo mengi ya ndani na nje ya mpira naona mabadiliko katika uchezaji wangu wa mpira" amesema Uhuru.
Ameendelea kusema "hapo nyuma nilikata tamaa kutokana na hata viongozi walikuwa hawanithamini hasa baada ya kuumia goti na nilipoelekea India kufanyiwa upasuaji lakini sasa najiamini na ninacheza mpira, kwahiyo namuona Phiri kama mzazi wangu"  
Rockersports ilifanya mahojiano maalum na kocha Phiri juu ya uwezo wa Uhuru wa Uhuru Selemani ambaye alimsifia winga huyo kwa kusema kwasasa amerejea na kwamba anamtegemea kubadilisha hali ya mchezo uwanjani kwa kuwani anamtumia kama mchezaji huru anapokuwa uwanjani.
"uhuru ni mchezaji huru uwanjani ni mzuri anapokuwa anaingia tunapokuwa tumeshindwa plan ya kwanza namtegemea sana kikosini hasa tunapokuwa tunataka kuwachanganya wapinzani"
Uhuru Selemani alirejea Simba akitokea Coastal Union ya Tanga kabla ya kuanza kwa mzunguko wa wa pili wa ligi msimu uliopita kuanza.
Kabla ya kujiunga na Coastal alikuwa akiichezea Azam fc ambako alihamia kwa mkopo akitokea Simba ambayo ilimuacha kutokana na kutokuwa fiti kwa aslimia mia moja baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti nchini India.

No comments:

Post a Comment