Simbu alivyojitabiria kutwaa dhahabu miaka 8 iliyopita
Mara ya kwanza aliposhika viatu vya riadha akiwa kijana mdogo huko Singida, hakuwahi kudhani kwamba baada ya miaka miwili baadaye angekuwa shujaa wa taifa lake na bara la Afrika.
Septemba 15, 2025, Alphonce Felix Simbu ameweka historia kwa kuwa Mtanzania wa kwanza kushinda medali ya dhahabu katika Mashindano ya riadha ya dunia.
Miaka minane iliyopita, katika mahojiano na BBC akieleza ndoto zake baada ya kufuzu kwa mara ya kwanza kushiriki mashindano ya dunia, Simbu alisema kwa kujiamini: "naiona dhahabu itakuja." Sasa kauli hiyo imekuwa unabii uliotimia, baada ya ushindi wa Tokyo 2025.
"Sikuwa najua ningeshinda, lakini nilipoona kwenye skrini ya TV uwanjani kwamba mstari wa kumaliza hauko mbali, nikasema uuh nikazane! Nashukuru nimetengeneza historia, hakuna Mtanzania aliyewahi kushinda medali ya dhahabu", anasema Simbu baada ya kuweka historia.
Simbu aliyezaliwa tarehe 14 Februari 1992 wilayani Ikungi, mkoa wa Singida, alianza riadha akiwa shule ya msingi kwa kujifurahisha na kwa mapenzi kama ilivyo kwa wanamichezo wengine akifanya mazoezi ya kawaida na marafiki zake.
Kwa Hisani ya Mtandao wa BBC Swahili
.jpeg)
Post a Comment