Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, September 26, 2014

RAUNDI YA NNE CAPITAL ONE CUP: MAN CITY vs NEWCASTLE, LIVERPOOL vs SWANSEA, STOKE vs SOUTHAMPTON, SHREWSBURY vs CHELSEA


Frank Lampard akishangilia goli lake la tatu katika mechi mbili dhidi ya Sheffield jana

SHREWSBURY Town, timu pekee ya daraja la chini zaidi iliyosalia katika michuano ya kombe la ligi 'Capital One Cup' amepangwa kukutana na timu ngumu ya ligi kuu ya England, Chelsea kwenye mechi ya raundi ya nne.
Raundi iliyopita Shrews inayocheza daraja la pili iliwaondoa mabingwa wa Championship, Norwich na sasa itawakaribisha Chelsea walioshinda 2-1 dhidi ya Bolton jana usiku.
Mabingwa watetezi, Manchester City, walioitoa Sheffield jana kwa kuifunga mabao 7-0 katika dimba la Etihad watachuana na Newcastle inayocheza ligi kuu.
Liverpool waliosonga mbele kwa penati 14-13 dhidi ya Middlesbrough jumanne usiku, watachuana na Swansea City, zote zinacheza ligi kuu.
Stoke wataikaribisha Southampton , wakati Tottenham watakuwa nyumbani dhidi ya Brighton.
Mechi nyingine za raundi ya nne zitawakutanisha Sheffield United watakaosafiri kuifuata MK Dons na Fulham watakabiliana na Derby.


Capital One Cup:
MECHI ZA RAUNDI YA NNE
Tottenham Hotspur vs Brighton
Stoke vs Southampton
Bournemouth vs West Brom
Shrewsbury vs Chelsea
Liverpool vs Swansea
MK Dons vs Sheffield United
Manchester City vs Newcastle United


Suso wa Liverpool (kulia) akishangilia goli lake la penalti dhidi ya Middlesbrough

No comments:

Post a Comment