Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, July 28, 2014

NEW YORK RED BULLS YAIFUNGA ARSENAL 1-0.

Wright-Phillips aliwafungia bao la pekee  New York Red Bulls dakika ya 32 na kuwapatia ushindi wa Bao 1-0 walipocheza na Arsenal huko Red Bull Arena, Harrison, USA.
Kwenye Mechi hiyo, Nguli wa Arsenal Thierry Henry aliichezea Klabu yake New York Red Bulls na Kona iliyopigwa na yeye ndio iliyozaa Bao baada ya Ibrahim Sekagya kupiga Kichwa na Bradley Wright-Phillips kukwamisha Mpira wavuni.
Bradley Wright-Phillips ni Mdogo wake Mchezaji Shaun Wright-Phillips wa QPR na ni Watoto wa Staa wa zamani wa Arsenal, Ian Wright.
Arsenal walianza Mechi hii bila Sentafowadi yeyote anaetambulika na hilo liliwafanya kushindwa kusumbua Difensi ya Bulls.


Kipindi cha Pili, Arsenal walibadilika walipomtoa Kiungo Mikel Arteta na kumwingiza Sentafowadi halisi Chuba Akpom na hapo ndipo wakapata nafasi kadhaa za kufunga.
Kipigo hiki kimeweka Rekodi kwa kuifanya Arsenal iwe Timu ya Kwanza kutoka England kufungwa na Klabu inayocheza MLS, Major Legue Soccer, ya huko Marekani ya Kaskazini.
Lakini Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amejitetea: “Ni gemu yetu ya kwanza na ilikuwa ngumu kinguvu hasa baada ya Wachezaji kurudi Mazoezini hivi karibuni, wengine walianza Juzi tu!”
Santi Cazorla dhidi ya Ambroise OyongoKipa wa New York Red Bulls  Luis Robles akikumbatia mpira mbele ya  Jack Wilshere.Henry  akikwaana  na WilshereMfungaji wa Bao  Bradley Wright-Phillips akigombea mpira wa konaAaron Ramsey alitupwa chini na  Tim Cahill.Kipa wa Arsenal Wojciech Szczesny akinyaka mpira mbele ya adui.Cahill akichuana na mchezaji wa  Arsenal Gedion Zelalem
VIKOSI:
New York Red Bulls (4-4-1-1):
Robles (Meara 81); Duvall (Kimura 77), Olave (Armando 46), Sekagya (Miazga 61), Miller (Alexander 46); Sam (Lade 81), Cahill (Bustamante 62), McCarty (Bover 70) , Oyongo; Henry (Luyindula 54); Wright-Phillips (Akpan 46).
Subs (not used): Castano, Eckersely, Obekop, Stevenson.
Goals: Wright Phillips 33'

Arsenal (4-3-2-1): Szczesny (Martinez 46); Jenkinson (Bellerin 46), Hayden (Miquel 46), Monreal, Gibbs; Arteta (Diaby 46), Wilshere (Coquelin 46), Ramsey (Flamini 46); Zelalem (Akpom 46), Cazorla (Olsson 71 ); Rosicky (Toral 71).
Attendance: 25,219

No comments:

Post a Comment