Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, July 24, 2014

MATUKIO MBALIMBALI KABLA YA KUANZA KWA MICHEZO YA JUMUIYA YA MADOLA

 

Masihara: Prince Charles na Camilla wakiongea na wachezaji wa mchezo wa badminton wa Wales alipotembelea Emirates Arena na Chris Hoy Velodrome mjini Glasgow
Zaidi ya watu bilioni duniani kote wanatazamiwa kuangalia sherehe za ufunguzi wa mashindano ya 20 ya Jumuiya ya Madola uwanja wa Celtic Park, ambayo waandaaji wamesema itakuwa ni ya kufana sana kuwahi kutokea nchini Scotland. Waimbaji Rod Stewart, Susan Boyle na Amy Macdonald ni miongoni mwa watakao tumbiza mbele ya watazamaji 40,000. 
Malkia kiongozi wa nchi za Jumuiya ya madola anatazamiwa kuhudhuria sherehe akiwa na Duke wa Edinburgh kwa ufunguzi rasmi wa tukio hilo kubwa kabisa kwa mwaka huu wa 2014.
Final preparations: Celtic Park goes through the motions ahead of the ceremony, which has been described as most prestigious live event Scotland has ever seen
Maandalizi ya mwisho: Celtic Park unazidi kupendeza kuelekea kwenye ufunguzi wa michezo ya Madola ambayo imeelezewa kuwa itakuwa ni babukubwa.
Head-to-head: Fans of different teams gather at Celtic Park before the 20th Commonwealth Games opening ceremony kicks off
Uso kwa uso: Mashabiki wa mataifa mbalimbali wakiungana kwa pamoja Celtic Park kabla ya ufunguzi rasmi wa michezo ya 20 ya Madola 2014.

Travelling support: A group of Team England fans are in high spirits at Celtic's 40,000-seater stadium ahead of the glittering opening ceremony
Mashabiki: Kikundi cha ushangiliaji cha England wakiwa katika morali ndani ya uwanja wa Celtic wenye uwezo wa kuchukua watu 40,000 kwa mara moja kabla ya ufunguzi wa Madola.
In the spotlight: Three Team Scotland fans wearing viking helmets with the Saltire on joke around in the sunshine at Celtic Park
Mashabiki wa Scotland wakiwa na kofia na skafu ndani ya Celtic Park


Fancy a fight? Prince Charles jokingly spars with a member of the Jamaican Commonwealth Boxing Team as he visits the Emirates Arena and Chris Hoy Velodrome
Prince Charles akitaniana na wachezaji wa Jamaican wa jumuiya ya Madola wa mchezo wa ngumi alipotembelea Emirates Arena na Chris Hoy Velodrome
Excitement: Long queues at the Commonwealth Games Ticket Office in Glasgow City centre ahead of the opening ceremony
Ni maandalizi tu na hali ya kusisimua katika mji wa Glasgow wakati wakati wa utafutaji wa tiketi

MASHINDANO YA JUMUIYA YA MADOLA YAFUNGULIWA RASMI HII LEO

Michuano ya jumuia ya Madola kwa mwaka 2014, imefunguliwa rasmi hii leo jijini Glasgow nchini Scotland huku mataifa 71 yakitarajiwa kushindana katika michezo 17 tofauti, ambayo itaanza kutimua vumbi lake kesho.

Tayari waziri mkuu wa nchini Scotland, Alex Salmond ameshathibitisha kukamilika kwa maandalizi ya michuano hiyo ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu kubwa na wadau wa michezo duniani kote, huku kila nchi ikiamini wawakilishi wao wataibuka na medali ima za dhahabu, shaba ama fedha.

Salmond amewataka wachezaji kutoka kila kona ya dunia kujihisi wapo nyumbani na washiriki michuano hiyo kwa amani ambayo itafikia tamati August 3.
Hata hivyo kiongozi huyo amewasihi wanamichezo watakaoshiriki michuano ya Jumuia ya Madola kwa mwaka huu huko mjini Glasgow, kujiepusha na kadhia ya kutumia dawa za kuongeza nguvu michezoni, ili kuepuka balaa ambalo huenda likawaharibia maisha yao ya baadae katika nyanja ya kimichezo.

Amesema vipo vinywaji vya kawaida ambavyo vinatumika na vinaruhusiwa kwa wanamichezo kuvitumia wakati wote, lakini wasithubutu kwenda nje ya maadili kwa kunywa vinywaji ama dawa zenye chembe chembe za kuongeza nguvu.

Waziri mkuu wa nchini Scotland, Alex Salmond.

Michezo itakayoshindaniwa katika michuano ya jumuia ya madola kwa mwaka huu ni Kurusha tufe, riadha, mbio za baiskeli, masumbwi, kuogelea, kuchupa kwenye maji, Judo, mpira wa pete, Rugby, mpira wa meza, kunyanyua vitu vizito, mieleka, Squash, Sarakasi, mpira wa magongo, kulenga shabaha pamoja na Badminton.

No comments:

Post a Comment