Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, February 21, 2014

MICHAEL LAUDRUP: NILITIMULIWA KWA BARUA PEPE

MENEJA wa zamani wa klabu ya Swansea City, Michael Laudrup amedai kuwa alitimuliwa kwa barua pepe saa chache baada ya kuambiwa kibarua chake kiko salama na kushikana mikono na mwenyekiti wa klabu hiyo Huw Jenkins. Laudrup mwenye umri wa miaka 49 aliiongoza klabu hiyo kunyakuwa Kombe la Ligi msimu uliopita likiwa ni taji la kwanza kubwa kwa timu hiyo katika hitoria yao ya miaka 102. Hata hivyo alitimuliwa mwezi huu baada ya matokeo mabovu ya timu hiyo na kutokuelewana kwa benchi lake la ufundi. Kocha huyo amesema jambo hilo la kutimuliwa kwa kupewa barua pepe lilimchanganya sana kwani lilitokea muda mchache baada ya kuhakikishiwa kibarua chake huku akipeana mkono na Jenkins. Laudrup ambaye pia amewahi kuinoa Real Mallorca ameendelea kudai kuwa alifanya mazungumzo na Jenkins na kumtaka kufukuza benchi lake la ufundi lakini alimkatalia hatua ambayo ilipelekea kutimuliwa siku moja baadae.
Wachezaji wa Swansea wakiwa wamebeba kombe la Capital One Cup msimu uliopita mwezi Februarikwa sasa ni Garry Monk

No comments:

Post a Comment