Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 22, 2014

KOCHA WA MAN CITY MANUEL PELLEGRINI ASHITAKIWA NA UEFA BAADA YA TIMU YAKE KUFUNWA BAO 2-0 NA BARCELONA, AKIMTUHUMU MWAMUZI JONAS ERIKSSON

Kocha Manuel Pellegrini
UEFA imemfungulia Mashitaka Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini kwa matamshi yake mara baada ya Timu yake kufungwa 2-0 na FC Barcelona Jumanne iliyopita Uwanja wa Etihad kwenye Mechi ya UCL, UEFA CHAMPIONS LIGI.Pellegrini alimponda vikali Refa kutoka Sweden, Eriksson, na kudai Refa huyo hakuwa na msimamo wa kutopendelea Timu moja.Jana Pellegrini aliomba radhi kwa kubatuka baada ya Mechi lakini hilo halikumsaidia kwani UEFA imemfungulia Mashitaka na shauri lake litasikilizwa na Bodi ya Nidhamu ya UEFA hapo Februari 28. 
Mara baada ya Mechi hiyo ya Man City na Barcelona ambayo Barca walipata Bao lao la kwanza kwa Penati ya Lionel Messi baada ya yeye mwenyewe kuchezewa Rafu na Martin Demichelis, ambae alipewa Kadi Nyekundu kwa tukio hilo, Pellegrini alikasirishwa kwa Penati hiyo huku kukiwa na madai kuwa Rafu yenyewe ilikuwa nje ya Boksi.

Patashika kwenye lango la Barca!

Barca walifunga Bao la Pili katika Dakika ya 88 kupitia Dani Alves na Timu hizi zitarudiana huko Nou Camp hapo Machi 12. Akiongea na Wanahabari baada ya Mechi hiyo, Pellegrini alisema: “Nina malamiko, si Penati tu na Kadi Nyekundu. Katika Mechi nzima hatukuwa na Refa aliechezesha Mechi sawa kwa pande zote!”
Joe Hart of Manchester City reacts after Lionel Messi of Barcelona scored the opening goal from a penalty kick during the UEFA Champions League Round of 16 first leg match between Manchester City and Barcelona at the Etihad Stadium on February 18, 2014 in Manchester, England.
Aliongeza: “Aliamua Gemu. Aliamua Mechi kwa sababu ilikuwa faulo ya Sergio Busquets kwa Navas. Refa alikuwa Mita 3 tu na hakupiga filimbi na baada ya hapo ile faulo ya Demichelis ilikuwa nje ya Boksi, hivyo si Penati. Makosa makubwa kwa Timu kama Barca yanafanya iwe ngumu kushinda!”
Pellegrini alienda mbali zaidi na kudai kuwa Refa Jonas Eriksson hakupaswa kupewa Mechi hiyo na UEFA kwa sababu alishawahi kukwaruzana na Barcelona Mwaka 2012 kwa kuwanyima Penati kadhaa walipocheza na AC Milan huko San Siro na kutoka 0-0 kwenye Raundi ya Mtoano ya UCL.

Mwaka huo, Kocha wa Barca wakati huo, Pep Guardiola hakulalamika chochote, lakini Magazeti ya Spain yalikerwa sana na kumsakama Refa Eriksson.
Hata hivyo, Barca walishinda Mechi ya Marudiano huko Nou Camp Bao 3-1.

No comments:

Post a Comment