Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, December 9, 2013

RATIBA: UEFA CHAMPIONS LEAGUE LEO JUMANNE: RAUNDI YA MTOANO - MECHI ZA MWISHO ZA MAKUNDI, MAN UNITED vs SHAKHTAR DONETSK, GALATASARAY vs JUVENTUS, BAYERN MUNICH vs MAN CITY...JUMATANO NI NAPOLI vs ARSENAL..



Hatua ya Makundi inafikia tamati Wiki hii, leo Jumanne na kesho Jumatano, kwa Mechi za mwisho na tayari Timu 8 zimejihakikishia kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na bado zipo Nafasi 8.
Timu 8 zilizofuzu ni Mabingwa Watetezi Bayern Munich, Chelsea, Manchester City, Manchester United, Real Madrid, Paris St-Germain, Barcelona, na Atletico Madrid.
Arsenal, licha ya kushinda Mechi 4 kati ya 5 katika Kundi F, bado wanangoja uhakika kwa matokeo ya Mechi yao ya mwisho Ugenini huko Italy na Napoli.



Kocha wa United David Moyes akiwa mazoezini kujiweka sawa na Uefa Champions League mchezo wa marudiano na Shakhtar Donetsk mchezo utakaopigwa leo jumanne usiku.

Robin van Persie anatarajia kucheza mechi hii wakati United watakapominyana na Shakhtar Donetsk

Pamoja na Moyes timu yake kuchapwa na timu ya Everton na Newcastle bado anajipa matumaini ya timu yake kujiweka sawa zaidi ili kuwa kwenye nafasi yake ya juu kwenye ligi kuu England

Leo kwenye mazoezi Moyes akiangalia vijana wake wanavyojifua tayari kwa kucheza na Shakhtar Donetsk

Antonio Valencia, Anderson, Wayne Rooney na Phil Jones wakifanya mazoezi Carrington

Tom Cleverley, Darren Fletcher, Adnan Januzaj na Fabio nao wakipasha hapa!!

Rio Ferdinand katikati wakijifua kujiweka sawa na Donetsk leo jumatatu

Robin van Persie na Wayne Rooneywakiteta jambo huku Van Persie akijipa moja zaidi kwa kusema yeye na Rooney wakiambatana vizuri wataiwezesha timu yao kuwa katika nafasi nzuri na kuondoa ukame wa mabao kati yao na timu.

Kinda Adnan Januzaj akimkimbiza kumkaba Wayne Rooney kulia...

Kocha wa Manchester United manager David Moyes akiwacheki vijana wake hapa

Darren Fletcher nae alikuwepo kwenye mazoezi hayo!

Wayne Rooney

Moyesakiangalia chini...sijuhi anawaza nini!!!nafasi aliyopo kwenye Ligi kuu au?

MECHI ZA MWISHO ZA MAKUNDI.
Jumanne 10 Desemba 2013
Manchester United FC v FC Shakhtar Donetsk
Real Sociedad de Fútbol v Bayer 04 Leverkusen
Galatasaray v A.Ş. Juventus
FC København v Real Madrid CF
SL Benfica v Paris Saint-Germain
Olympiacos v FC RSC Anderlecht
FC Bayern München v Manchester City FC
Viktoria Plzeň v PFC CSKA Moskva

Jumatano 11 Desemba 2013
FC Schalke 04 v FC Basel 1893
Chelsea FC v FC Steaua Bucureşti
Olympique de Marseille v Borussia Dortmund
Napoli v Arsenal FC
FK Austria Wien v Football Club Zenit
Club Atlético de Madrid v FC Porto
AC Milan v AFC Ajax
FC Barcelona v Celtic Fc

No comments:

Post a Comment