Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, September 30, 2013

BALE ALIMBANIA SIGURDSSON KUTUA SUNDERLAND, EVERTON YAPANIA KUMBAKIZA BARRY, FLETCHER KURUDI UWANJANI OCTOBA NA MUSTAKABALI WA TERRY MIKONONI MWA MOURIHNO



LONDON, England
STRAIKA wa Tottenham Hotspur, Gylfi Sigurdsson (24), alishindwa kutua Sunderland akitokea Spurs kutokana na sakata la uhamisho wa Gareth Bale kwenda Real Madrid, inasemekana Sigurdsson ambaye alifunga bao la Spurs kwenye sare ya bao 1-1 dhidi ya Chelsea, alitakiwa na Sunderland na jamaa walikuwa tayari kutoa pauni milioni 10 kwa ajili yake, lakini kampuni yake ya uwakala ya Stellar Group ilikuwa imeelekeza nguvu zake zote kufanikisha uhamisho wa Bale na kumsahau yeye.
@@@@

Everton wapania kumbakiza Barry
LIVERPOOL, England
EVERTON wanataka kumpa mkataba wa kudumu, Gareth Barry (32), anayeichezea klabu hiyo kwa sasa kwa mkopo wa muda mrefu akitokea Manchester City, inasemekana kocha wa miamba hiyo ya Goodison Park, Roberto Martinez, ameridhishwa na kiwango cha nyota anayepokea kiasi cha pauni 120,000 (sh milioni 304.363) kwa wiki na anataka kumbakiza baada ya mkataba wake wa mkopo kuisha.
@@@@
 
Fletcher kurudi uwanjani Oktoba
MANCHESTER, England
KIUNGO wa Manchester United, Darren Fletcher (29) anatarajiwa kurudi uwanjani Oktoba, mwaka huu baada ya kukaa benchi kwa muda mrefu akisumbuliwa na majeruhi, bado haijafahamika siku rasmi ambayo Fletcher atarudi uwanjani, lakini madaktari wa Man Utd wanaamini itakuwa Oktoba, hii ni baada ya kukaa benchi tangu Januari, huku katika kipindi cha miaka miwili akicheza mechi saba tu, kutokana na matatizo ya kiafya.
@@@@

Mustakabali wa Terry mikononi kwa Mourinho
LONDON, England
MUSTAKABALI wa John Terry (32), katika klabu ya Chelsea, uko mikononi kwa kocha wake, Jose Mourinho, ambaye ndiye ameshika rungu la kuamua kumuongeza mkataba au kumuacha aende zake pindi mkataba wake wa sasa utakapomalizika. Zamani Mkurugenzi wa Ufundi, Michael Emenalo na Bodi ya klabu ndiyo walikuwa na sauti ya kuamua, lakini sasa hivi Mourinho ndiye mwenye sauti ya mwisho kwenye ishu ya Terry na Frank Lampard.

No comments:

Post a Comment