Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, September 30, 2013

SMS YA MESSI ILIMTIMUA IBRAHIMOVIC CAMP NOU, KAGAWA NJIA PANDA MAN U NA WENGER AHAMIA KWA LARS BENDER


BARCELONA, Hispania
IMEFAHAMIKA kwamba, meseji ya Lionel Messi kwa kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola, ndiyo iliyomfukuzisha Zlatan Ibrahimovic Camp Nou.
Katika kitabu cha El Misterio de Messi (Upande wa pili wa Messi), waandishi Sebastian Fest na Alexandre Juillard wametoboa siri za tabia mbovu za Messi.
Sehemu ya kwanza ya kitabu hicho iliyopewa jina la El Shock, imeeleza jinsi Messi alivyochangia kumuondoa Ibra, Camp Nou, inasemekana baada ya Ibra kusajiliwa mwaka 2009, Messi aliamua kumuandikia sms Guardiola ambayo ilikuwa inasema: “Sawa bwana, ninaona kwamba sina umuhimu tena kwenye timu, hivyo…..”
Sms hiyo ya Messi inasemakana kumfanya Guardiola ambaye alilazimisha uhamisho wa Ibra kuanza kutaka kumtumia pembeni Ibra, lakini Msweden huyo aligoma na kuamua kuondoka msimu uliofuata.
@@@@
 
Kagawa njia panda Man Utd
MANCHESTER, England
MUSTAKABALI wa Shinji Kagawa, Manchester United unaonekana kuwa njia panda, kutokana na staa huyo wa Kijapan kutolewa wakati wa mapumziko kwenye mechi dhidi ya West Brom ambayo United ililala kwa mabao 2-1, lakini David Moyes mwenyewe anadai kuwa alimtoa Kagawa kutokana na sababu za kiufundi, na kusisitiza kwamba Mjapan huyo yupo kwenye mipango yake ya baadaye.
@@@\
 
Wenger ahamia kwa Lars Bender
LONDON, England
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger anaonekana kuanza kunogewa na wachezaji wa Kijerumani, baada ya kumsajili Mesut Ozil na sasa chaguo lake la kwanza kwenye usajili wa wakati wa Januari ni kiungo wa Bayer Leverkusen, Lars Bender na Wenger yuko tayari kuweka mezani pauni milioni 20 (sh bilioni 50.727).
Wenger tayari alishaweka mezani pauni milioni 18.5 (sh bilioni 45.654), kwa ajili ya kiungo huyo ambaye anatazamiwa kuja kurithi mikoba ya Mikael Arteta, huku kukiwa na taarifa kwamba Ozil ndiye aliyempigia debe Mjerumani mwenzake huyo.

No comments:

Post a Comment