![](http://garsoornews.com/news/wp-content/uploads/2013/07/zlatan-ibrahimovic.jpg)
BARCELONA,
Hispania
IMEFAHAMIKA kwamba, meseji ya Lionel Messi kwa kocha wa
zamani wa Barcelona,
Pep Guardiola, ndiyo iliyomfukuzisha Zlatan Ibrahimovic Camp Nou.
Katika kitabu cha El Misterio de Messi (Upande wa pili wa
Messi), waandishi Sebastian Fest na Alexandre Juillard wametoboa siri za tabia
mbovu za Messi.
Sehemu ya kwanza ya kitabu hicho iliyopewa jina la El Shock,
imeeleza jinsi Messi alivyochangia kumuondoa Ibra, Camp Nou,
inasemekana baada ya Ibra kusajiliwa mwaka 2009, Messi aliamua kumuandikia sms
Guardiola ambayo ilikuwa inasema: “Sawa bwana, ninaona kwamba sina umuhimu tena
kwenye timu, hivyo…..”
Sms hiyo ya Messi inasemakana kumfanya Guardiola ambaye
alilazimisha uhamisho wa Ibra kuanza kutaka kumtumia pembeni Ibra, lakini
Msweden huyo aligoma na kuamua kuondoka msimu uliofuata.
@@@@
Kagawa
njia panda Man Utd
MANCHESTER, England
MUSTAKABALI wa Shinji Kagawa, Manchester United unaonekana
kuwa njia panda, kutokana na staa huyo wa Kijapan kutolewa wakati wa mapumziko
kwenye mechi dhidi ya West Brom ambayo United
ililala kwa mabao 2-1, lakini David Moyes mwenyewe anadai kuwa alimtoa Kagawa
kutokana na sababu za kiufundi, na kusisitiza kwamba Mjapan huyo yupo kwenye
mipango yake ya baadaye.
@@@\
Wenger
ahamia kwa Lars Bender
LONDON, England
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger anaonekana kuanza kunogewa
na wachezaji wa Kijerumani, baada ya kumsajili Mesut Ozil na sasa chaguo lake
la kwanza kwenye usajili wa wakati wa Januari ni kiungo wa Bayer Leverkusen,
Lars Bender na Wenger yuko tayari kuweka mezani pauni milioni 20 (sh bilioni
50.727).
Wenger tayari alishaweka mezani pauni milioni 18.5 (sh
bilioni 45.654), kwa ajili ya kiungo huyo ambaye anatazamiwa kuja kurithi
mikoba ya Mikael Arteta, huku kukiwa na taarifa kwamba Ozil ndiye aliyempigia
debe Mjerumani mwenzake huyo.
No comments:
Post a Comment