Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, June 25, 2013

WANASOKA MAARUFU NCHINI WAHITIMU KOZI YA UKOCHA YA NGAZI YA KATI LEO

Picha ya pamoja ya wahitimu wote







Seleman Matola akipongezwa

Kulia Suleman Matola wa Simba, Rahel Pallangyo, Zuberi Katwila wa Mtibwa na Steven Nyenge mchezaji wa zamani wa Simba



Rahel Pallangyo ambaye pia ni mwamuzi na mwandishi wa habari alikuwa mhitimu pekee wa kike




Golikipa wa zamani wa Simba Moses Mkandawile akipongezwa na Tenga




RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodger Tenga, amewataka makocha kuhakikisha wanaibua vipaji vya watoto ili kuwa na vipaji vingi baadaye.

Tenga ametoa rai hiyo kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam leo, wakati akifunga kozi ya siku 21 ya makocha wa mchezo huo ngazi ya pili, iliyoandaliwa na Chama cha Mpira wa Miguu Dar es Salaam (DRFA), huku ikishirikisha zaidi ya makocha 58.

Tenga amesema Bara la Afrika ndilo bara lenye upungufu mkubwa wa wachezaji watoto, tofauti na mabara mengine, kitu ambacho kinarudisha nyuma maendeleo ya soka.

“Hili ndilo bara ambalo lipo nyuma katika kuibua vipaji, mfano nchi ya Ujerumani pekee ina watoto zaidi ya milioni  moja ambao wanaandaliwa, lakini hapa sijui kama wanafika hata idadi hiyo, hivyo kuna changamoto kubwa katika hilo,” alisema.

Amewataka kuhakikisha wanayatumia mafunzo hayo katika kuleta mabadiliko katika soka hapa nchini, ambapo pia aliwapongeza kwa kushiriki katika kozi hiyo.

Naye Mkurugenzi wa Ufundi wa DRFA, Joseph Kanakamfumu, alisema kozi hiyo imefanyika kwa mafanikio makubwa, kwani walimu wote walikuwa wasikivu na wameweza kupata mafunzo ya kutosha.

“Tunashukuru Chama cha Makocha Tanzania (TAFCA) kwa kuwezesha wakufunzi ambao waliweza kuendesha mafunzo haya, lakini pia walimu hawa waliojitokeza tunawashukuru,” alisema.

No comments:

Post a Comment