Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 30, 2013

TORRES ATAKIWA ARSENAL AKACHEZE SAMBAMBA NA GONZALO HIGUAIN

London, England

KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho anaamini kuwa wachezaji watano katika Kikosi chake cha Stamford Bridge, ndiyo wenye uhakika wa kupata nafasi ya kuanza, jambo linalomfanya amkubalie Arsene Wenger kumpigia kasi Mhispania, Fernando Torres.

Bosi huyo wa Arsenal, Wenger anaitaka huduma ya Torres Emirates, wameripoti Dean Jones na Dave Kidd wa Gazeti la The Sunday People.

Hata hivyo, Mourinho yupo tayari kumruhusu Mhispania huyo kuondoka baada ya kubainika kuwa katika mipango yake, hadi sasa wachezaji wenye uhakika wa kuanza kwenye kikosi chake ni Petr Cech, Ashley Cole, Frank Lampard, Eden Hazard na Oscar.

Mchezaji mwenye Kipaji raia wa Hispania, Juan Mata na Beki wa Kati wa Kimataifa wa Brazil, David Luiz pia si miongoni mwa watakaounda kikosi chake, hivyo watapewa mkono wa kwaheri majira haya ya joto. Mourinho anaamini Oscar anastahili kucheza namba 10, kutokana na kuwa bora kuliko Mata.

Lakini hizo ni taarifa nzuri kwa Arsenal ambayo imejipanga kuelekea kwa Torres, ambaye wanaamini ataweza kutengeneza kombinesheni nzuri Emirates akicheza sambamba na Mshambuliaji wa Real Madrid, Gonzalo Higuain wanayetarajia kumsajili.

Bodi ya The Gunners ipo tayari kuona timu yao ikisajili nyota wengi, baada ya hivi karibuni kushuhudia wachezaji wao wenye majina makubwa wakiihama klabu hiyo.

Torres, ambaye yupo Brazil kwa majukumu ya kitaifa ambapo timu yake, Hispania jana ilicheza mechi ya fainali ya Kombe la Mabara dhidi ya wenyeji hao, hana uhakika kama yupo kwenye mipango ya baadaye ya Chelsea, hivyo anatarajia kuzungumza na Mourinho wiki hii na Arsenal itampigia kasi 'fasta' kama atatemwa.

Chaguo la kwanza kwa Arsenal ni Higuain, lakini Torres na Wayne Rooney wa Man United pia wapo katika mipango yao.

Katika hatua nyingine, Mourinho sasa atahitaji kusajili wachezaji sita kabla ya dirisha la usajili kufungwa na anatambua wazi kuwa, pauni milioni 35 atakazozipata kutokana na kumuuza Luiz kwa Barca, zitamtosha kuboresha kikosi chake.


Nyota wa Brazil, Hulk anayeichezea Zenit St Petersburg, Mario Gomez wa Bayern Munich na Mshambuliaji wa AC Milan, Stephan El Shaarawy wote wapo katika rada za Mourinho, sambamba na Kifaa cha Manchester City, Edin Dzeko.

No comments:

Post a Comment