Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 30, 2013

OKWI APATA SOKO ULAYA HUKU MSIMBAZI MAMBO YAKIZIDI KUNOGA

SIMBA imecheza rafu, baada ya kuzuia mikataba ya nyota watano wa Yanga, kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Hatua hiyo, inatokana na wachezaji hao ambao ni Frank Domayo, Simon Msuva, Kelvin Yondani, Ally Mustapha ‘Barthez’ kuanza mazungumzo na viongozi wa Simba.

Wachezaji hao ambao wamo kwenye kikosi cha timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, inadaiwa wamekataa kuendelea kuichezea Yanga pindi mikataba yao itakapomalizika.

Domayo ambaye ni kiungo tegemezi katika Kikosi cha Yanga na Stars, alijiunga na timu hiyo katika msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara akitokea JKT Ruvu na Msuva Moro United, kisha kusaini mkataba wa miaka miwili kila mmoja.

Kwa upande wa Yondani na Barthez, walijiunga na timu hiyo wakitokea Simba  katika msimu uliopita na kuiwezesha timu hiyo kuchukua ubingwa wa ligi kuu.

 Habari zilizopatikana kutoka ndani ya uongozi wa Simba, zilieleza kwamba, wachezaji hao wameonyesha nia ya kutaka kuichezea timu yao ya zamani, wakiamini wataweza kufikia malengo waliyojiwekea ya kucheza soka katika klabu kubwa za Afrika na Ulaya.

Chanzo hicho kilieleza kwamba, wanachosubiri wachezaji hao kwa sasa ni kumaliza mikataba yao ili waweze kusaini Simba, hasa wakizingatia baadhi yao ni wanachama hai wa klabu hiyo.

Kilieleza kwamba, wachezaji hao wameona Simba ni klabu pekee inayoweza kuwauza na wakacheza soka kwa mafanikio makubwa kama ilivyokuwa kwa wenzao, Mbwana Samatta na Emmanuel Okwi.

Samatta aliuzwa na Simba katika misimu mitatu iliyopita ya Ligi Kuu Tanzania Bara, katika Klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya kung’ara katika michuano ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho barani Afrika, ambapo Okwi aliuzwa Etoile de Sahel ya Tunisia ambaye sasa anatarajiwa kuuzwa Ulaya katika Klabu ya Partizan Beograd ya nchini Serbia.

Taarifa zilizolifikia zilidai kuwa Etoile de Sahel ipo katika mazungumzo na klabu hiyo ya Serbia, ambayo inataka kumsajili Okwi baada ya kumvutia Kocha wao, Vuk Rasovic.

Partizan Beograd imetwaa ubingwa wa Serbia msimu uliomalizika baada ya kumaliza ligi hiyo inayoshirikisha timu 16 ikiwa na pointi 73, zikiwa ni pointi 11 mbele ya Crvena Zvezda iliyomaliza ya pili na 12 dhidi ya Vojvodina Novi Sad ambayo imeshika nafasi ya tatu.


Chanzo hicho kilieleza kwamba, wachezaji wengi wanaounda kikosi cha kwanza cha Yanga kama Mrisho Ngassa, Athumani Idd ‘Chuji’, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Yondani na Barthez na Kipa mpya wa timu hiyo, Deogratius Munishi ‘Dida’ ni wanachama hai wa Klabu ya Simba

No comments:

Post a Comment