Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 30, 2013

KIBADENI AANZA TAMBO MSIMBAZI


NILETEENI Yanga muone kazi yangu! Hivyo ndivyo unaweza kusema baada ya Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah ‘King’ Kibadeni, kusema vijana wake wameiva kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Simba katika msimu uliopita ilipokea kipigo cha mabao 2-0, katika mchezo wa marudiano wa Ligi Kuu uliochezwa Mei 18, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ikiwa chini ya Kocha Mkuu wake, Mfaransa, Patrick Liewig.

Lakini Kibadeni ameanza kujiamini mapema kuwa kikosi chake kinaweza kubadilisha matokeo ya msimu uliopita, baada ya kujiridhisha vijana wake wameiva kwa ajili ya ligi hiyo.

 Akizungumza Dar es Salaam jana, Kibadeni alisema kutokana na uwezo uliooneshwa na vijana wake  kwa takribani mwezi mmoja katika mazoezi yanayoendelea kwenye Uwanja wa Kinesi, hana shaka kabisa ya kuanza kwa ligi hiyo.

Kibadeni alisema vijana wake wapo tayari kucheza, ingawa anaendelea na mazoezi makali ya kuwajengea nguvu ya mwili  katika Gym ya Chang’ombe na baadaye mazoezi ya kawaida Uwanja wa Kinesi.

Kibadeni alisema anajivunia timu hiyo, kwani inaundwa na wachezaji wengi chipukizi licha ya kuwemo wengine wakongwe kama Nassor Masoud ‘Chollo’, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Musa Mude, Abel Dhaira na Haruna Shamte.

Alisema hana hofu kabisa kuhusu kutemwa kwa kipa na nahodha wa timu hiyo, Juma Kaseja kwa kuwa anao makipa watatu katika kikosi chake, akiwemo Andrew Ntalla aliyesajili msimu huu, akitokea Kagera Sugar.

Kikosi kipya cha timu hiyo kinaundwa na wachezaji  Zahor Pazi, aliyesajiliwa kutoka (Azam FC), ambaye msimu uliopita alikuwa akicheza kwa mkopo katika klabu ya Ruvu Shooting na Augustino Sino (Tanzania Prisons).

Wengine ni Kipa Andrew Ntalla (Kagera Sugar), Samuel Ssenkoom (URA ya Uganda), Adeyoon Salehe (Miembeni ya Zanzibar), Ibrahim Twaha ‘Neymar’ (Coastal Union) na Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ (Mtibwa Sugar).

Kadhalika wamo, Shomari Kapombe, Kiemba, Kazimoto, Chollo, Salum Kinje, Haruna Shamte, Mude na Dhaira huku akiwapandisha wachezaji wengi wa kikosi cha pili cha timu hiyo, Miraji Adam, Hassan Khatib, Willian Lucas, Daid Ndemla, Abdallah Seseme, Hassan Isihaka, Marcel Kahenza, Ramadhan Singano ‘Messi’, Haruna Chanongo, Jonas Mkude, Christopher Edward, ambao baadhi yao walipandishwa katika misimu miwili iliyopita.



No comments:

Post a Comment