Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, May 27, 2013

SHIRIKA LA NYUMBA LAINGIA MIKATABA NA BENKI TANO LEO KWA AJILI YA MIKOPO YA NYUMBA KWA WATEJA


CEO wa DCB Edmund  Mkwawa (kushoto) akisani makubaliano na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Felix Maagi baada ya kuingia makubaliano ya mkopo wa nyumba kwenye hafla iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam. 




Mkurugenzi Mkuu wa BancABC, Boni Nyoni (kushoto) akipeana mkono na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Felix Maagi baada ya kuingia makubaliano ya mkopo wa nyumba kwenye hafla iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam







CEO wa MGen Tanzania Charles Sumbwe akibadilisha faili na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Felix Maagi baada ya kuingia makubaliano ya mkopo wa nyumba kwenye hafla iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. 

Viongozi wa benki za DCI, NIC, CRDB, BancABC na MGen Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kutia saini makubaliano

Viongozi wa mabenki na shirika la Nyumba wakiwa kwenye picha ya pamoja





Wadau wakifuatilia kwa makini jinsi mambo yanavyokwenda
BENKI nne za jijini Dar es Salaam, zimesaini makubaliano na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa ajili ya kuwakopesha wananchi fedha za kununulia nyumba zinazojengwa na shirika hilo.
Makubaliano hayo yalisainiwa jijini Dar es Salaam leo kati ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NHC, Felix Maagi na viongozi wakuu wa benki hizo.

Benki zilizosaini makubaliano hayo ni DCB, ABC, NIC pamoja na Benki ya CRDB.
Akizungumza wakati wa makubaliano hayo, Maagi alisema yamefanyika kama sehemu ya mwendelezo wa taasisi za fedha kushirikiana na NHC kuwafanya wananchi wamiliki nyumba.
“Kama mtakumbuka, mwaka juzi tulisaini makubaliano na mabenki manane kwa ajili ya kuwasaidia wananchi kuweza kumiliki nyumba.

“Kwa faida ya wale ambao hawakuwapo wakati tunasaini makubaliano ya kwanza, ni kwamba tulisaini na Benki za Azania, BOA, CBA, Exim, KCB, NBC, NMB na Benki ya Stanbic.
“Kwa maana hiyo, kitendo cha kusaini makubaliano na mabenki haya manne leo ni mwendelezo wa utaratibu wetu wa kushirikiana na taasisi za fedha katika kuwakomboa wananchi, hasa hasa katika umiliki wa nyumba,” alisema Maagi.     

Kwa mujibu wa Maagi, lengo la shirika hilo ni kuwafanya wananchi waachane na tabia ya upangaji, badala yake wawe na uwezo wa kumiliki nyumba zinazojengwa na kuuzwa na shirika hilo kupitia mikopo inayotolewa na benki mbalimbali.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Bima ya MGen Tanzania, Charles Sumbwe, ambaye kampuni yake imesaini mkataba na NHC kwa ajili ya kuwadhamini wananchi wa kipato cha chini ili nao waweze kumiliki nyumba, alisema kampuni yake imelazimika kusaini mkataba huo, baada ya kuguswa na tatizo la wananchi wengi kutokuwa na uwezo wa kumiliki nyumba.
“Moja ya majukumu ya kampuni yetu ni kuwasaidia wananchi, kwa hiyo, tumeamua kujitosa katika kuwadhamini wananchi wenye uwezo mdogo kifedha ili nao waweze kumiliki nyumba kama ilivyo kwa wenye nazo,” alisema Sumbwe

No comments:

Post a Comment