Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, March 11, 2013

NI ISSA HAYATOU TENA CAF

RAIS wa Shirikisho la Soka Barani Afrika-CAF, Issa Hayatou amechaguliwa tena bila kupingwa kuendelea kushika wadhfa huo kwa kipindi cha miaka mingine minne. Katika uchaguzi huo Danny Jordaan ambaye alijitengenezea jina kubwa kimataifa baada ya kuandaa michuano ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini mwaka 2010 ameshindwa kwa mara nyingine kupata nafasi ya ujumbe katika kamati ya utendaji ya CAF. Jordaan alishindwa na mgombea kutoka Madagascar aliyetumia jina moja la Ahmad katika uchaguzi hiyo ikiwa mara ya pili kukosa nafasi hiyo nyeti baada ya mara ya kwanza kugaragazwa katika mkutano uliofanyika nchini Sudan miaka miwili iliyopita. Katika mkutano huo uliofanyika jijini Marrakech nchini Morocco aliyekuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka la Dunia-FIFA Amadou Diakite alichaguliwa kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya CAF. Diakite alifungiwa na FIFA kwa miaka miwili Novemba mwaka 2010 baada ya kutuhumiwa kupokea rushwa katika skendo ya kununua kura uliozunguka nchi zilizopewa uennyeji wa kuandaa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 na 2022. Shirikisho hilo linatarajia kufanya mkutano mwingine nchini Brazil mwaka 2014 lakini kutakuwa hakuna uchaguzi tena mpaka mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment