Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, March 17, 2013

MSHINO FC YATWAA UBINGWA WA LIGI DARAJA LA NNE YA MANISPAA YA IRINGA

Aliyekuwa katibu wa shirikisho la soka nchini TFF Fredrick Mwakalebela akimkabidhi kombe la ubingwa wa soka Iringa mjini nahodha wa timu Mshindo pamoja na fedha taslimu shilingi laki tano kufuatia kutwaa ubingwa wa ligi ya Iringa mjini katika uwanja wa Samora. Timu ya magereza ilishika nafasi ya pili na kuzawadiwa shilingi laki tatu.

Mwakalebela akitoa neno la kwa mashabiki wa soka wa Iringa mjini wakati wa kukabidhi zawadi kwa washindi wa ligi ya Iringa Mjini jioni ya leo.,

Hizi ni baadhi ya zawadi kwa washindi.

Hapa akizikagua timu za Mshindo na Magereza.





















 


 


TIMU ya Mshindo FC jana iliibuka mabingwa wa ligi daraja la nne wilaya ya Iringa Mjini baada ya kuifunga Magereza mabao 3-2 na kufanikiwa kuondoka na Kombe na kitita cha shilingi laki tano kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Samora mjini Iringa.
Mchezo huo ambao ulivuta hisia za mashabiki wa mji wa Iringa ulishuhudia Mshindo wakienda mapumziko wakiongoza kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na Abdallah Mativila dakika ya 27 na 30

Kipindi cha pili kilianza kwa timu kufanya mabadiliko na Magereza walipata bao kupitia kwa John Ngairo dakika ya 65  bao ambalo halikudu muda mrefu kwa Abdallah Mativila aliongeza bao la tatu kwa Mshindo dakika ya 78 na John Ngairo wa Magereza aliongeza bao la pili dakika ya 80.
Magereza ambao ni washindi wa pili waliondoka na zawadi ya lakini tatu na mshindi wa tatu Mtwivila City walizawadiwa shilingi laki mbili

Mlinda lango bora Sunday Mwakasala alipewa zawadi ya shilingi elfu hamsini wakati mfungaji bora  Kasim Mataka alifunga mabao 18 alipewa shilingi elfu 80. Wakati timu yenye nidhamu, Uhuru FC ilipata laki moja.

Akizungumza na Mtanzania kwa njia ya simu toka Iringa, Katibu wa chama cha Soka Rashid Shungu alisema anashukuru Ligi imemalizika salama na mshindi amepatikana.

 

No comments:

Post a Comment