Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, February 5, 2013

CAMEROON WANASEMA WAKO TAYARI KWA MCHEZO WA KESHO NA STARS NAO WATAONYESHA KIWANGO KAMA ILIVYO ILIVYOKUWA KWA ZAMBIA.

Meneja wa timu ya taifa ya Cameroon Rogobart Song akiongea na waandishi wa habari juu ya mchezo wa kesho.
Kocha mkuu wa timu ya taufa ya Cameroon Akono Jean Paul akionegela maandalizi yake kwa mchezo wa kesho dhidi ya Stars kubwa ni kwamba anaiheshimu taifa stars kutokana na kwamba mpira wa miguu Afrika unafanana lakini pia kutokana na matokeo ya mchezo uliopita dhidi ya Zambia.
Kutoka kushoto ni katibu mkuu wa shirikisho la soka nchini TFF Angetilile Oseah, kocha msaidizi wa Cameroon Ndtoungou Martin, nahodha wa meneja wa Cameroon Robert Song na kocha wao  Akono Jean Paul wakati wa mkutano na waandishi wa habari.
Hapa wakisikiliza maswali ya waandishi wa habari wa mwisho kulia ni nahodha msaidizi Wome Nlend Pierre .
Nahodha Wome Nlend Pierre akifuatilia maswali ya waandishi wa habari.
Katibu mkuu wa TFF Angetile Oseah leo aligeuka kuwa mkalimani kwa kutafsiri lugha ya kifaransa kurahisha mawasilino baina ya kocha Akono wa Cameroon kwa waandishi wa habari.
Kutoka kushoto ni Angetile Oseah, kocha stars Kim Poulsen na nahodha Juma Kaseja wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika ofisi za TFF.
Kocha Kim Poulsen akisisitiza kuwa anaimani Stars itafanya vizuri kwani maandalizi ni mazuri na kwamba atawatumia Mrisho Ngasa na Mbwana Samata pembeni kwa lengo la kupata kasi ya mchezo lakini akitaka mchezo wa pasi na kasi na kujiamini.

No comments:

Post a Comment