Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, January 30, 2013

LULU AKIWA NA USO WA MACHOZI YA FURAHA BAADA YA KUACHIWA

Msanii  Elizabeth "Lulu" Michael tayari amerudi uraiani baada ya kuachiwa kwa dhamana katika mahakama kuu jijini Dar. Licha ya kukamilisha kwa masharti yote aliyopewa jana ikiwa ni pamoja na kutoa milioni 20 kwa wadhamini wawili, kuripoti kila mwanzo wa mwezi na kuacha hati yake ya kusafiria mahakamani hapo, Lulu hakufanikiwa kutoka kwa kile kilichoripotiwa kutokuwepo kwa msajili , hivyo kumlazimu kurudi gerezani

Lulu (katikati) akiwa mwenye majonzi na furaha hapa akitokwa na machozi wakati msemaji wa familia Msanii Dr Cheni akizungumza . Lulu amewaomba watanzania wote wamuombee maana hii ni dhamana tu na kesi yake bado inaendela.


LULU na Mama yake mzazi ndani ya gari tayari kwa safari ya kurudi nyumbani
Wakili wake Ndugu Flugence Massawe amesema kwamba hii ni hatua ya kwanza kwasababu case bado inaendelea. Kwa sasa wanasubiri mahakama itoe tarehe ya Lulu kurudi mahakamani.

No comments:

Post a Comment