Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, December 26, 2012

YANGA YALEWESHWA NA TUSKER MOJA UWANJA WA TAIFA BAADA YA KUKUBALI KICHAPO

Klabu bingwa nchini Kenya Tusker  leo imefanikiwa kuifunga klabu bingwa Afrika mashariki na kati, Yanga ya Tanzania kwa bao 1-0 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
  
Bao la Tusker lilipatikana katika dakika ya 44 ya mchezo likifungwa na Ismail Dunga kwa njia ya penati baada ya mwamuzi Oden Mbaga kuamuru penati iliyotokana na kiungo Nurdin Bkari kumwangusha katika eneo la hatari Aucho Khali.

Katika mchezo huo  Yanga inayofundishwa wa kocha wake Ernstus Brands iliwatumia wachezaji wake watatu iliyo waongeza katika usajili wa dirisha dogo akiwemo Kabange Twite na wachezaji vijana waliopandishwa kutoka kikosi cha pili Rehani Kibingu na George Banda ambao walionyesha uwezo wa kuridhisha licha ya kucheza kipindi cha kwanza kabla ya kutolewa mapumziko.

Kipindi cha pili licha ya Yanga kuwaingiza Hamisi Kiiza, Jerson Tegete, Omega Seme na Nizar Khalfani akichukua nafasi za George Banda, Rehani Kibingu, Ladslaus Mbogo, Saidi Bahanuzi na David Luhende bado matokeo ya mchezo huo yalisalia kama ilivyokuwa kipindi cha kwanza ingawa mabadiliko hayo yalibadilisha sura ya mchezo kwa Yanga kufanya mashambulizi kadhaa langoni mwa Tusker katika dakika za mwisho wa mchezo huo

Baada ya mchezo huo Yanga sasa inajiwinda na safari ya wiki mbili nchini Uturuki ikiwa sehemu yake ya maandalizi ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara, safari ambayo imepangwa kufanyika kabla ya mwaka mpya.Tusker ilingara na wachezaji wake kama George Opiyo, Luke Ochieng, Joseph Shikokoti, Ismail Dunga na Robert Omonuk.

No comments:

Post a Comment